Nyota Ndogo Aajiri Mrembeshaji Binafsi Baada Ya Masaibu Ya Vipodosi Katika Harusi Yake


Taarifa za harusi yake zilipogonga vichwa vya habari, kilichoongelewa sana ni jinsi hitmaker huyo wa Watu Na Viatu alivyokua amepodolewa visivyo.
Wengi waliweza kukosoa jinsi alivyokua amepakwa make up siku ya harusi wakisema ya kwamba ilikua haiendani na rangi ya ngozi yake na alikua anatisha.
Tukio kama hilo huenda lisiwahi tokea tena kwani kuanzia hivi sasa, Nyota Ndogo ameajiri mrembeshaji binafsi ambaye atakua anamshuhulikia kuhusu mavazi na vipodozi katika kila tamasha atalokua anahudhuria, si Kenya tu bali hadi nje ya nchi.

Kupitia Beryl Kawere, ambaye ni brand ambassador wa LAVIES SPA & BARBERSHOP (0720 325 364/ 0735 010 780 ) Nyali,  ambaye alikua harusini kwa Nyota Ndogo, aliweza kumualika Nyota Ndogo Katika salon hio na akafanyiwa make up na kurembeshwa nywele wakati wa photoshoot ya project yake inayokuja hivi karibuni.

Nyota Ndogo alifurahishwa na kazi ya stylist huyo, Braxton #Tha_SalonGuybrax na akaamua ya kwamba huo ndio mwanzo mpya wa hao wawili kufanya kazi kwani yeye ndiye atakaye kua stylist wake, sio tu katika maisha yake ya kawaida bali pia katika kila tamasha atakalo kua anaenda, iwe nchini au nje ya nchi, braxton ndiye atakaye shuhulikia maswala ya Nyota Ndogo ya urembo.

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele