Posts

Showing posts from February, 2015

NEW TRACK:SUSUMILA FT SARKOZY-IHALE

Image
BONYEZA HAPA KUSKIZA LISTEN

CHIDI BENZ AOKOLEWA NA MAMA YAKE

Image
Rapper mkali kutoka mtaa wa ilala Dar rees salam Chid Benz aepushwa kifungo cha miaka miwili gerezani na mama yake.Rapper huyo siku ya alhamisi alikua amehukumiwa kifungo cha miaka miwili gerezani au alipe  f aini ya shillingi laki saba za tanzania ambapo mamake alimlipia faini hiyo iliyomuweka chidi huru uraiani tena. Hukumu hiyo ilitolewa  baada ya  chidi kupatikana na hatia ya makosa matatu ikiwemo kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroin yenye thamani ya sh. 38, 638, bangi yenye thamani ya sh. 1,720 na  vifaa ya kuvutia dawa hizo.Mnamo  Februari 18 Chidi Benz aliwahi  kukiri makosa yote matatu mbele ya Hakimu.

NEW MUSIC:PASS K FT SWAHIB-MCHUMBA

Image
Skiza na kudownload wimbo mpya wa msanii kutoka studio ya Crack sound kilifi kwa jina pass k akiwa amemshirikisha swahib.Wimbo wenyewe unaenda kwa jina la mchumba na umetayarishwa na producer j crack.Pass k ni msanii ambaye amewahi kutamba na vibao kama vile tatizo la moyo,nakufuata na fadhila vyote akimshirikisha shaah biggy. DOWNLOAD

MSANII SUSUMILA AFUNGUKA KUHUSU MIPANGO YAKE YA MWAKA WA 2015

Image
Huenda ukawa una maswali mengi kuhusu ukimya wa Msanii kutoka pwani Susumila ambaye kwa sasa anatamba na ngoma ya Hidaya.Susumila amefunguka mengi saana kumhusu  katika kipindi cha Sifa paradise ndani ya Sifa f.m ikiwemo malengo yake ya mwaka wa 2015,kuhusu ngoma yake mpya ambayo anatarajia kuiachilia ijumaa 27/2/2015,wasanii ambao atashirikiana nao,pamoja na uhusiano wake na aliyekua producer wake TK2.Kwa yote haya na mengi zaidi bonyeza link iliyopo hapo chini kumsikiliza msanii huyo moja kwa moja katika mahojiano yake ndani ya kipindi cha sifa paradise na Mp kelvin jilani DOWNLOAD

MSANII CHEGE AKANUSHA MADAI YA KUVAA HIRIZI STEJINI

Image
Msanii    kutoka katika kundi la Wanaume Family  Chege Chigunda amejitokeza na kukanusha tetesi zilizoenea kuhusu picha yake anayoonekana amevaa kitu kinachofanana na hirizi katika mkono wake wa kushoto.Msanii huyo kutoka kundi la TMK amewashukia kwa ukali waandishi waliosambaza uvumi huo nakuweka wazi  kuwa alichokua amekivaa sio hirizi  bali ni kitu alivaa katika msiba wa msanii Mez B. "Ushamba+roho mbaya+uandishi bila kusomea ni hatari sana hahaaahahahahahhaa eti waandishi magumashi wanadai nimevaa hirizi hahahhaaaaa hii tulivaa juzi dodoma siku ambayo alifariki msanii mwenzetu marehemu Mez B,msiwe vimbele mbele"

VIDEO MPYA YA RABBIT AKIMSHIRIKISHA RICH MAVOKO

Image