Posts

Showing posts from February, 2016

Donde Samora Ajitosa Kwenye Siasa

Image
Ni mtangazaji wa redio mkongwe hapa mkoani. Alianza kupata umaarufu mwaka wa 2000 alipojiunga na Baraka FM. Mwaka wa 2004 alijiunga na Pwani FM , kituo cha redio kinachomilikiwa na Shirikika La Utangazaji Kenya(KBC) hio ilikua ni kabla ya kujiunga na Pilipili FM Mwaka wa 2013. Ikiwa ni mda ambao watu wanajitayarisha na uchaguzi wa mwakani, watu wengi wameonyesha azma yao ya kuwania vyeo mbalimbali katika uchaguzi ujao. Donde naye hajaachwa nyuma kwani hapo jana, Jumapili ya 28 Februari, akihudhuria misa katika kanisa la katoliki Juda , Donde alitangaza rasmi ya kwamba anajitosa katika ulingo wa kisiasa na anapania kupigania kiti cha MCA , wodi ya Junda. Donde alisistiza ya kwamba maamuzi yapo mikononi kwa wananchi ya ni wajibu wa kila mwananchi ahakikishe ya kwamba amejisajili kama mpige kura ili ifikapo katika uchaguzi awe na uwezo wa kufanya maamuzi kwa kuchagua viongozi wanaostahili.

NEW MUSIC: Harmonize Ft Diamond Platnumz-BADO

Image
Kutoka Wasafi Classic Records , hawa hapa ni CEO wa wasafi, Diamond Platnumz akiwa ameshirikishwa na kijana ambaye amem,sign na ameweza kuonyesha uwezo mkubwa sana baada ya kuteka anga za mziki na track yake ya kwanza kutoka Wasafi ya AIYOLA. Hiki hapa ni kichupa kipya ambacho Harmonize amemshirikisha boss wake. DOWNLOAD / LISTEN HERE

Kumbe Kigoto hutangaza mechi za Soccer

Image
Ni msanii ambaye ana uwezo mkubwa sana wa utunzi. Ukitengeneza orodha ya wasanii hapa nyumbani ambao wanapeta sana kwenye anga za mziki ukikosa kum,weka basi hio list itabidi itengenezewe kamati ili kuichunguza. Ali,hit sana na Kichapo Cha Mapenzi na baadae hit kama vile Ridhika, Vumilia na Aire akiwa Number1 Records chini ya uongozi wa Produecr TK2 . Hio ni kabla kuhamia Nairobi ambako ana management mpya ambayo chini ya uongozi wake aliachia track na video ya Hello Hello mwishoni mwa mwaka jana. Lakini kando na mziki, kumbe Kigoto ni mkali sana katika utangazaji wa soka.... Yani hata hahitaji mashabiki kwani anaweza piga kujazia tu mwenyewe zile shangwe za mashabiki. Usidhani ni porojo zangu tu...Huyu hapa Kigoto akifanya mambo yako Bonyeza Hapa Kumskiliza Kigoto

NEW VIDEO: Nay Wa Mitego- SHIKA ADABU YAKO

Image
Ni track ambayo iligonga vichwa vya habari tu baada ya kuachiwa kwani kama kawaida yake, Nay alikua ameongea vitu controversial sana kama vile kuhoji uhakika wa mimbo ya Wema Sepetu ambayo baadae aliipoteza, tetesi za kwamba Ommy Dimpoz 'hapigi mechi'. .. Ni track ambayo hata BASATA aliipiga marufu na kumkataza Nay kutoiongelea katika vyombo vya habari kwani hata hao walikua wamechanwa hatika track hio. Hatimaye video imedondoshwa ikiwa imeongozwa na NICKLASS....  

Baada Ya Kukaa Kimya Kwa Mda Mrefu , Peter Adamz Arudi Hewani

Image
usibonyeze hicho kidude ..... msemo wake maarufu anaopenda kuutumia akiambia mashabiki wake waendelee kumtegea. Peter Adamz au ukipenda P.A ni mtangazaji aliyetambulika sana kwa kucheza mziki wa hapa nyumbani na sanasana chipukizi enzi zile akiwa Pwani FM. Lakini baadae alijiunga na Radio Maisha ambako pia alikua na kipindi cha Tv kwa mda mfupi katika runinga ya KTN-Iz Vipi XL Mashariki. Hio ilikua kabla kuhamia Radio Jambo ambako alikaa tu kwa mda mfupi alafu akapotea hewani katika hali tatanishi. Lakini hatimaye P.A amevunja ukimya na kutangaza ya kwamba anarudi hewani katika Radio Jambo. Kupitia account yake ya Facebook, alipost:

Unamjua Sis Shanniez? Je ushawahi kumuona akiwa kazini? hii hapa ni fursa yakipekee ya kukujuza

Image
Anaitwa Sis Shanniez aka Anti Viru s, majina aliobatizwa katika mwezi wake wa kwanza alipofanya kipindi kutokana na misimamo yake mikali kuhusu tasnia ya mziki kanda ya pwani.Ni mtangazaji wa kipindi cha Kaya Flavaz,  kila siku jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa tatu asubuhi kipindi ambacho kinapeperushwa katika Radio Kaya- 93.1 fm msa, 99.7 fm mlnd, 94.9fm voi ,   kituo ambacho makao yake makuu yako mjini Kwale.  Amekua kwenye tasnia ya utangazaji kwa mda wa miaka 5. Anajulikana sana kwa kuwa presenter mwenye msimamo asiyeyumbishwa kirahisi na kuwa na msimamo thabithi katika vitu anavyotaka kufanya.  Jambo ambalo wengi hawajui kuhusu Sis Shanniez , dada ambaye ana mapenzi mengi na sanaa ya hapa pwani na anajifua sana kuona ya kwamba sanaa ya mziki hapa nyumbani inaendelea ni kwamba ana dada mmoja tu mdogo ambaye anampenda sana. Wengi wamekiri ya kwamba wanatamani sana kumuona Shanniez akiwa kazi, na kama shukrani kwa mashabiki wake wanaomuunga mkono kazi yake na kumpa

Artiste To Watch This year

Image
Hassan Salim ndio jina lake halisi lakini katika sanaa anajulikana kama Kelechi Africana . Ni chipukizi ambaye aliachia wimbo wake wa kwanza huu mwaka lakini ameshangaza wengi kwa uwezo wake mkubwa alio nao kiasi ya kwamba ukimuita chiopukizi ni kama wamuonea vile.Ana style unique ya mziki ambayo yeye mwenyewe anaiita AfriNAIJA , styl ambayo anachanganya kizungu, kiswahili, kimijikenda na mahadhi ya kinaijeria. Aliachia wimbo wake wa kwanza kwa jina Bomboribo mwishoni mwa Januari na baadae aliashirikishwa katika wimbo For Me wa Alyento . Kwakua ana bidii ya kazi na meneja wake ambaye ni Athman Babaz ameamua Africana ni kazi tu mwenda mbele na mwaka ni track tu baada ya track,mwezi huu wa   Februari, Kelechi akishirikiana na Wasojali Band waliachia wimbo kwa jina Nitalia Nawe ambao umetokea kupendwa sana na unapeta sana katika chati za mziki hapa pwani. Nitalia Nawe ndio project ambayo ataifungulia mwezi wa March kwani ndio video yake itakapokua inadondoshwa na mwezi h

NEW MUSIC: GZee Feat Kimbo-VIDONGE VYAO

Image
Hassan Juma aka GZee ni msanii kutoka mji wa Malindi anayefanya mtindo wa RnB na Hiphop . Japo anatokea Malindi, mishemishe zake za mziki huzifanyia mjini Kilifi katika studio ya Jay Crack, Crack Sounds Records. Afisaa huyu wa usalama mwaka jana aliachia wimbo aliomshirikisha Shaa Biggy kwa jina Hisia Kali na sasa amerudi tena na VIDONGE VYAO raundi hii akiwa amemshirikisha mkali wa kuchana Master Kimbo.   DOWNLOAD / LISTEN HERE

Susumila Aongelea Kuhusu Ndoa, Track 3 ambazo zilimuinua sana mwaka jana na mambo mengi kumhusu

Image
Susumila alifunguka na kusema ya kwamba kando na kufanya track 12 mwaka jana, kuna track 3 ambazo zilimpa mafanikio makubwa sana kwenye mziki. Susumila alikiri ya kwamba yeye kujaaliwa mke mwema mwaka jana ndio ilikua achievement kubwa sana mwaka jana, alisema ya kwamba Ihale, Tuliza Nyavu na KideKide ndio track ambazo zilimuinua sana katika sanaa ya mziki mwaka jana. Kuhusu mapokezi kwa mashabiki wake mwaka huu, Susumila ameweka wazi shukrani zake kwa mapokezi mazuri ya track kali aliyofanya na msanii wa nairobi KAKA SUNGURA inayokwenda kwa jina la mapepe. Kulingana na Susumila, mapokezi mazuri ya track hiyo haswa katika miji ya Mombasa na Nairobi yanampa kila sababu ya kuamini kuwa mwaka huu tayari umeanza vizuri kwa upande wake. Susumila amesema kuwa kwa sasa tayari yeye na msanii mwenzake kaka sungura wako mbioni kuandaa utayarishaji wa video ya wimbo wa Mapepe ambayo wanapania ku shoot tarehe 10 mwezi ujao jijini Nairobi. Msanii huyu ambaye aliandikisha ma

NEW VIDEO: Dogo Richie -YOYOBA

Image
YOYOBA ni track ambayo iliandaliwa na Producer Totti ambayo Dogo Richie aliidondosha mwishoni mwa mwaka jana na bado inatamba katika maredio na mitaani. Mwaka ukianza Dogo Richie aliahidi ya kwamba huu mwaka ni kuuza sura kwa sana, akimaanisha ya kwamba atadondosha video nyingi mno, hii ni baada ya yeye ku,sign,iwa na KingKong Entertainment. Na akiionyesha seriousness ya kauli yake ameanza na video timam kabisa ya Yoyoba ikiwa imeongozwa na Lil Guy G.  

Shirko anastahili kutambuliwa kwa kuchangia kutangaza Mombasa nchini Tanzania, asema Amoury

Image
Msanii huyo mkongwe wa mombasa amejitokeza na kusema kuwa producer shirko ni moja kati ya ma producer ambao hawajapata heshima wanayostahili.Kulingana na amour ni kwamba kufikia sasa wadau wa mziki wanafaa kutambua kazi kubwa anayoifanya shirko ikizingatiwa kuwa kufikia sasa producer huyo ametayarisha hits kali saana za kundi la ya moto band ambalo limetikisa afrika mashariki kwa mda sasa.."yamoto band kwa sasa wako juu,sasa kwanini watu watambue ya moto band na wasimtambue shirko ambaye ametayarisha nyimbo zao,kama tanzania wanamtambua mbona sisi kama watu wa mombasa tusimtambue"alisema Amoury.   Mbali na hayo Amoury pia amezungumzia baadhi ya miradi ambayo shirko anatarajia kuifanya mombasa,vipi je kuhusu SAV CLAN pamoja na alipo VICTOR MO,VIBES RECORDS pamoja na ujio wake mpya na malengo ya kampuni yao ya kutayarisha videos. Kwa mengi zaidi Bonyeza HAPA kumskliza akifunguka

NEW MUSIC: Cannibal, Susumila, Kaa Laa Moto, Vivonce-SUPERSTAR

Image
Mkongwe wa mziki wa HipHop Cannibal alipotea kwa mda mrefu sana katika game. Na hivi karibuni maekua akijifua sana kurudi kachukua nafasi yake katika mziki. Hajarudi katika mziki tu bali pia amejitosa katika siasa kwani anapigania kua MCA wa ward ya Kiembeni katika uchaguzi mwakani. Baada ya kumshirikisha Juma Nature katika Kidaluso, track ambayo inatesa sana katika chati za mda hivi sasa nchini Tanzania, hii ni mpya akiwa ameshirikiana na Vivonce, Susumila na Kaa Laa Moto , star mkali wa hiphop ambaye ameamua huu mwaka ni ma,collabo kwenda mbele ikiwa imetayarishwa na mikono ya Producer Amz, Tempoz. DOWNLOAD / LISTEN HERE  

DJ Kaytrixx Ajitosa Katika Siasa

Image
Uchaguzi unakaribia na watu wengi wa taaluma mbali mbali wameonyesha ari ya kuwania viti mbalimbali katika uchaguzi mwakani. Washikadau katika tasnia ya burudani pia hawajawachwa nyuma, kwani hapa pwani Cannibal na Mtaliano Eliano ni miongoni wa wasanii waliotangaza nia zao za kugombaia viti vya MCA . CEO wa Spin Cycle Entertainment Limited, DJ Kaytrix naye hajawachwa nyuma. Nyota yake ilianza kung'aa katika kinyang'anyiro cha “Pilsner Mfalme” mwaka wa 2008 wakati alipowakilishwa Pwani na kuebuka numba 5. Januari 2009 alijiunga na CodeRed kwa mda wa miaka miwili kabla kuanza kuwa binafsi mnamo 2011 na kuanzisha Dj Unit yake ya Spin Cycle Entertainment Limited ambayo ime,sign dj kama vile  Mr T, Xclusive, Bonez, Phauz na Scream . Kaytrixx ambaye amewahi kufanya show nyingi nchini Rwanda na Tanzania vilevile alitangaza ya kwamba anapania kuwania kiti cha MCA katika ward ya Mikindani katika uchaguzi wa 2017 . Akitangaza maamuzi hayo, Kaytrixx alihimiza watu

NEW VIDEO: Queen Renee- CHAMPAGNE

Image
Kutoka kwa Album yake ya pili inayoenda kwa jina CHAMPAGNE , hii ni track yake inayobeba jina la album hio. Queen Renee wikendi hii atakua nchini Ujerumani katika tamasha la Kenya Culture & Fashiona Show. Wimbo huu wa kujirusha na kusherehekea maisha umeandaliwa na Producer Akeem na video imetayarishwa na A-World Visuals.  

EXCLUSIVE MUSIC: Dazlah Feat Susumila-BANGEREBA REMIX

Image
Mwaka jana walifanya collabo ambayo ilitokea kua wimbo mkubwa zaidi kutoka pwani mwaka jana kwani wimbo huo ndio wimbo uliochezwa sana nchi nzima kutoka pwani. Kidekide ni wimbo ambao hata leo ni vigumu siku ikamilikie bila kuuskia wimbo huo kuchezwa katika redio au hata mix za ma,dj kwenye usafiri wa umma. Hii hapa ni remix ya Bangereba , track ambayo Dazlah alikua ameifanya 2014 peke yake. Na sasa amemshirikisha Susumila tena. Hili ni bonge la hit ambalo limetayarishwa na Producer Tee Hits na Producer Totti.   LISTEN/DOWNLOAD HERE    OR HERE

Barua Kwa ma,Presenter na ma,DJ kwa niaba ya Wasanii

Image
Juzi niliandika barua kwa wasanii kwa niaba ya Presenter na Dj , Leo nachukua fursa hii kuwakabidhi barua ma,presenter na ma,DJ kwa niaba ya wasanii maana mtaani kuna  lawama kibaoo....... Naelewa kuwa katika barua niliyoandika juzi nilisema kuwa kuchezwa kwenye redio sio haki ya msingi kwa msanii, ila hii haimaanishi kuwa napigia debe uozo ambao umeletwa na watangazaji na ma,Dj ambao kwa kiwango kikubwa sana wana nafasi kubwa sana katika tasnia ya mziki. Kwa kiwango kikubwa sana kifo cha mziki wa hapa nyumbani kinasababishwa na hawa wadau wawili DJ na PRESENTER. Hivi ni picha gani unayoipata Presenter anaijua historia yooote ya msanii Kanye West ila hatambui hata wasanii wawili wa nyumbani wanaotrend mtaani? Top ten chat ya radio station iko Mombasa imetawaliwa na nyimbo za Nigeria na marekani. Hivi inamaanisha nyumbani hakuna wasanii? Wasanii wengi wamelalamika kwamba katika baadhi ya vipindi wanalazimishwa kuhonga ndio nyimbo zao zichezwe hewani. Hivi ina maana

Dogo Richie & SimpleBoy-FOLLOW ME (Teaser)

Image
Mwishoni mwa wiki jana nilitembelea Studio ya Mo Fire Records , Mazeras na kwa bahati nzuri nlipata na hitmaker wa Yoyoba, Dogo Richie pamoja na SimpleBoy wakitayarisha track yao mpya kwa jina FOLLOW ME ambaye inatarajiwa kudondoka mda wowote kutoka sasa. Hiki hapa ni kionjo cha track hio kali ambayo imetayarishwa na Producer Tonniedadd. DOWNLOAD/LISTEN HERE  

NEW MUSIC: Queen Renee-KAMATA CHAMPAGNE

Image
Kutoka kwa Album yake ya pili ambayo inaitwa CHAMPAGNE huu ni wimbo wa 12 toka aanze mziki mwaka wa 2007. Kamata Champagne ni track ya kujirusha ambayo ilitayarishwa na Producer Akeem, Stubborn Records, Mtwapa. Akiachia track hii, Queen Renee alisema Ijumaa hii anaelekea Uswizi alafu aende Ujerumani wikendi hii kwa madhumuni ya kuend ku,perform katika tamasha la Kenya Culture & Fashiona Show. LISTEN / DOWNLOAD HERE  

NEW MUSIC: Wasojali Band & Kelechi Africana

Image
Walianza mziki mwaka jana wakiwa katika ulezi wa Athman Baba . Idris, Ability, Hamso na Jay Bro ambao ndio wanaounda kundi zima la WASOJALI BAND walikimbiza vizuri mwaka jana hadi kuchukua tuzo ya kundi bora  katika tuzo za Nzumari Award s. Huu mwaka nao wameamua kukimbiza zaidi kwani baada ya kuachia track yao mpya mwezi uliopita wamerudi tena wakiwa wamemshirikisha Kelechi Africana , chipukizi mwengine  mwenye talanta sana ambaye pia ako katika uangalizi wa Athman Baba. Hii ni track ambayo ilitayarishwa na Producer Noizer, GreenHouse Records. LISTEN / DOWNLOAD

Barua Kwa Wasanii Kwa Niaba Ya Mapresenter Na Ma,DJ

Image
Kama hadi sasa wewe ni msanii ambaye kila ukishuka unaelekeza lawama kwa Presenter au DJ nahisi ya kwamba itakua vizuri sana kama ungewacha mziki taratiiiiiibu na ujitaftie shuhli nyingine ufanye. Huu ni mtazamo wangu binafsi ila nahisi ni mtazamo ambao hata bila kupitishwa na mtu yoyote utakua una chembe chembe za ukweli ndani yake. Mimi binafsi huenda ikawa sijui changamoto wanazopitia wasanii ila kwa kiwango kikubwa saana nazielewa sana changamoto wanazozipitia haswa watang azaji .  Kwanza kabisa ukianza kulalamika kuhusu presenter flani kutocheza mziki wako jiulize kwanza presenter huyo kwa siku hupokea ngoma ngapi kwa e mail yake , pili jiulize je mziki wako una hadhi ya kutosha kuhimili ushindani uliopo, tatu je mziki wako una viwango vya kumletea faida na kumuongezea soko yule presenter au DJ katika kazi yake ? Ukishajiuliza maswali yote haya nahisi kwamba utapata jibu kwamba msanii na Presenter au DJ wanafaa kuwa na ushirikiano mkubwa sana ambao unaf

NEW MUSIC: Gaspery Feat Kigoto-SHANGINGI

Image
Gaspery Mwakatengo ambaye katika sanaa ya mziki anatumia jina Gaspery ni chipukizi ambaye anauwezo mkubwa wa kuchana na kuimba. Katika hii track yake ya kwanzaambayo inamtambulisha katika sanaa ya burudani Gaspery ame,rap na kuonyesha uwezo wake mkubwa wa utunzi na styl yake tofauti, amemshirikisha hitmaker, Kigoto. Track hii iliatayarishwa Number  1 Records na Producer mkali TK2. DOWNLOAD/ LISTEN HERE  

NEW MUSIC: Ohzy & Crazy K Feat Susumila-SHEREHE

Image
Ujio mpya wa Ohzy baada ya kukaa kimya kwa mda mrefu katika tasnia ya mziki, amerudi na hii ameshirikiana na Crazy K na Susumila . Ni track kali sana inayoongelea mambo ya kula bata, kujiachia na kusherehekea maisha. Ilitayarishwa na Producer Morbiz, Thundersounds Records. DOWNLOAD / LISTEN HERE

EXCLUSIVE VIDEO: Ohzy Feat Crazy K & Susumila

Image
Zile ngojangoja sasa kwishney , hatimaye ule ujio mpya wa rapper mkali Ohzy ndio huu. Kutoka ThurnderSounds Records kwa Producer Morbiz Sheriff, Susumila na Crazy K wameshirikishwa katika hii party Song, bonge la track. Video imetayarishwa na Ricky Bekko wa BigDreams Media.  

Kidis ajibu madai ya Kuzalisha mschana na kumtelekeza

Image
Baada ya mschana kwa jina Agnes kujitokeza na kusema ya kwamba muimbaji wa Viroboto alimpachika mimba na kumtelekeza yeye na mwamawe wa kike ambaye kwa sasa ana mwezi mmoja Kidis amefunguka kuhusu madai hayo. Kidis ambaye kwa sasa yuko nchini Tanzania , hapo Ijumaa alihojiwa na Gates Mgenge katika kipindi cha MashavMashav, Pwani FM kwa njia ya simu, alisema ya kwamba kama kuna yeyote ambaye ana uhakika ya kwamba ana mtoto wake basi amplekee kwani yeye hawezi kukataa damu yake. Gates alimuuliza iwapo anamjua Agnes na jibu la Kidis ilikua ya kwamba hamjui Agness lakini iwapo ana mtoto wake na ana uhakika ni wake ampelekee kwa kua hawezi kataa damu yake.

BASATA waufungiwa wimbo wa Nay WaMitego **Isome Barua Hapa**

Image
Mwanzoni BASATA ( Baraza la Sanaa la Taifa) walisema ya kwamba hawajaufungia wimbo wa Nay WaMitego-SHIKA ADABU YAKO mpaka pale watakapo maliza kufuata taratibu zote za kisheria. Na hatimaye hapo jana BASATA wakatoa barua kuufungiwa wimbo huo rasmi kwa madai ya kwamba wimbo huo una lugha ya maudhi,udhalilishaji,uchochezi n.k na kumpiga marufuku NAY kutouongelea wimbo huo popote kwenye vyombo vya habari.   Barua ya Basata hii hapa isome…. Ieleweke kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 4 (1) (j) cha sheria ya BASATA namba 23 ya mwaka 1984, Baraza limepwa mamlaka ya kuratibu na kufuatilia mienendo ya mtu yeyote anayehusika na kazi za Sanaa na kuhakikisha linalinda maadili ya kitaifa miongoni mwa Wasanii wanapokuwa jukwaani au wanapobuni kazi yoyote ya Sanaa. Aidha, kifungu cha 4 (2) cha sheria hii kinalipa Baraza nguvu ya kisheria kufanya jambo lolote lile kuliwezesha kufanya majukumu yake kwa faida na ustawi wataifa. Baraza la Sanaa la Taifa limekuwa likipokea simu za m

NEW MUSIC: AKA & Diamond Platnumz-MAKE ME SING

Image
Bonge  moja la Colabo kutoka kwa Diamond Platnumz akiwa ameshirikiana na AKA kutoka Afrika Kusini. Ni track ambayo ilitayarishwa na producer mkubwa kutoka Tanzania, Tuddy Thomas.   DOWNLOAD / LISTEN HERE

NEW MUSIC: BenPol Feat Jux-NAKUCHANA

Image
Kutoka AM Records, hawa hapa wasanii wawili wakali wa Rnb bongo, hitmaker wa Nikuite nani, Jux na star wa Sophia . Ni bonge la track ukizingatia ya kwamba wote wamezoea kuimba mapenzi lakini kwa hii ambayo wamefanya styl ya majibizano, hawahimba mapenzi bali muonekano wao wa mziki na ushindani wa binafsi kimziki, kama vile Jux kutwaa tuzo ya mwanamziki bora wa Rnb ambayo BenPol alikua ameitangulia kuikwarua. DOWNLOAD / LISTEN HERE