Posts

Showing posts from May, 2016

Kutoka Tutu Band Ilikua Maamuzi Yangu Binafsi, Sikulazimishwa na Nyota Ndogo, Tatu Afunguka

Image
Jina la msanii huyu mchanga lilijipata limezingirwa na utata wikendi iliyopita baada ya Juma Tutu ambaye ni kakake mkubwa kudai kuwa Tatu alikuwa amelazimishwa na dadake mkubwa ambaye ni Nyota Ndogo kutoka katika band ya Juma maarufu kama Tutu Band ambayo Tatu alikua akihudumu kama msanii pekee wa kike. Kulingana na Juma Tutu katika maandishi yake katika mtandao wa kijamii wikendi iliyopita ni kwamba nyota alimtoa Tatu katika bendi yake ili akamtaftie mume.Ilibidi tumtafute Tatu   ili tupate kujua ukweli wa ndani kuhusu madai yote haya na kwa bahati nzuri binti tulimpata na akaweka kila kitu wazi.... "mimi sio mtoto mdogo mimi ni msichana mkubwa na nina maamuzi yangu binafsi" Huyu hapa Tatu katika mahojiano na Kelvin Jilani/ MTU BEI ...msikilize akifunguka mengi yanayohusu mipango yake ya kimuziki huku akikuonjesha wimbo wake mpya ushuhudie utam wa sauti yake. Bonyeza  HAPA kusikiliza/Download

NEW MUSIC: Escobar Feat Kalicha - RIHOHO

Image
Zee La Kugandamaiza au ukipenda ESCOBAR , hitmaker wa Wanataka Kunijua ambaye wiki jana alitangaza ya kwamba amewacha masomo ili arudi katika mziki mzima mzima ameachia track ambayo inatambulisha ujio wake mpya. Escobar akiwa amemshirikisha Kalicha , ametayarishiwa track hii na Producer Noizer  wa GreenHouse Records. Liaten / Download HAPA  au  HAPA

Hiki Ndicho Kitakachotokea Baada Ya Nyota Kufunga Ndoa

Image
Mkongwe wa mziki hapa pwani, Nyota Ndogo aliweza kufunga pingu za maisha mwishoni mwa wiki jana na mchumba wake wa miaka miwili mwenye asili ya ki,dutch, Mr. Neilsen . Katika sherehe hio iliyohudhuriwa na ndugu, marafiki na baadhi na wasikadau katika tasnia ya mziki ilifanyika katika mkahawa wa RoseWood Hotel  mjini Voi . Neilsen ambaye ndio alikua anajishindia jiko siku hio anaonekana amenogewa na mapenzi si haba kwani katika sherehe hio, alisema ya kwamba baada ya kufunga ndoa na Nyota Ndogo , anajipanga kuhamia hapa nchini na kufanya Kenya kuwa makazi yake rasmi milele.

Nyota Ndogo Afunga Pingu Za Maisha **Picha Za Sherehe Hio**

Image
Ni mkongwe katika tasnia ya mziki wa hapa Pwani. Amekua katika fani ya mziki ya mziki kwa zaidi ya miaka 16. Hapo Jana, siku ya Jumapili iilikua siku ambayo ataienzi kwenye kumbukumbu zake kwani aliwezza kufunga pingu za maisha na mchumba wake wa miaka miwili, Nielsen mwenye asili ya ki,dutch. Sherehe hio ya Jumapili ndio ilikua kilele kwani ilikua imeanza siku ya jumamosi kwa harusi iliyofanywa ki,Islamu na sherehe hio ya Jumapili ilifanyika katika mkahawa wa RoseWood Hotel, mjini Voi. Ni sherehe iliyowezwa kuhudhuriwa na watu maarufu mbalimbali haswa katika tasnia ya mziki kama vile Esther ingolo, Sis Shaniez, Linnet Kanini, Hustla Jay, Johnny Skani, Beryl Kawere,  Kaa La Moto, Amourey Beyby, Lil Guy G, Hassan Faisal, Vivonce na wengine wengi. Tunamtakia kila la heri dada Nyota na Neilsen katika maisha yao mapya ya ndoa.

Ziki La Nazi Haikua Idea Yangu Lakini Tutumie Kama Identity Ya Mziki Wa Pwani, sistiz ALI B

Image
Kwa kipindi cha mda mrefu saana wasanii pamoja na wadau wa mziki wa pwani ya kenya wametafuta sana jina ambalo litakua nembo itakayobeba utambulisho wa mziki wa pwani. Mziki wa maeneo mengi umepata majina maalum kuutambulisha kwa mfano Nairobi kuna mziki mtindo wa Genge, Ghipuka, Kapuka huku Tanzania wakijivunia kutambulika na jina la Bongo Fleva .  Harakati za kuja na jina maalum litakalotambulisha mziki wa pwani ya kenya zimeonekana kuchipuka na kwa sasa kuna jina ambalo baadhi ya wasanii wameanza kulikumbatia. Msanii Ali B kwa kipindi cha mda sasa ameskika akitumia nembo ya "ZIKI LA NAZI" kwenye nyimbo zake huku akifikia kiwango cha kutoa wimbo uliobeba jina hilo.Ni nembo ambayo kufikia sasa wasanii kadhaa wameanza kuitumia na imeanza kukita mizizi.  Swali je nembo hii ilitokea wapi? Kulingana na Ali B sio yeye aliyebuni nembo hii....... "kusema kweli ziki la nazi tulikua tunazungumzia kuhusu jina litakalowakilisha mziki wetu,sasa katika meeting

Escobar Aacha Masomo Ili Kurudi Kwenye Mziki Fulltime

Image
Msanii Escobar mbaye siku za nyuma alisema kuwa amejipa likizo ya mziki kwa ajili ya kujipa mda kwenye Masomo kwa sasa amesema ameacha masomo na kurudi tena kwenye mziki. Kwa sasa msanii huyu yuko mbioni kuachilia ngoma yake mpya wiki ijayo ambayo amemshirikisha Kalicha .  Kwenye mipango na harakati zake za kurudi tena kwenye game na kupambana na ushindani uliopo,msanii huyu amekiri kuwa amelazimika kurudi kivingine kabisa ili alete utofauti katika style yake pamoja na kukidhi mahitaji ya soko la mziki kwa sasa.... " Zamani nilikua nikirap lakini siku hizi naimbaga saana kwa sababu mziki wa siku hizi ni wa kuimba saana, Rap inalipa lakini inabidi uiskume saana ndio itakulipa alafu isiwe hardcore" Escobar pia amesema kuwa amepanga kusafiri hadi nairobi kwa ajili ya kufanya remix ya wimbo wa yende yuye Bonyeza HERE kumsikiliza Escobar akifunguka.

Ali B Aeleza Siri Inayomfanya Kupata Dili Za Tamasha Kubwa Za Kitaifa

Image
Bila kupinga, Ali B ndiye msanii wa mziki wa kizazi kipya kutoka Pwani ambaye amewahi kutumbuiza katika tamasha nyingi za kitaifa kuliko msanii yeyote. Mbona yeye? Siri ni nini? Msanii Ali B amesema kua heshima ndio kiini kikubwa kinachomfanya anawakilisha na kukubalika na kila rika. Kulingana na Ali B ni kwamba heshima yake imemjengea brand kubwa kufikia kiwango cha kupewa heshima na fursa ya kuweza kutumbuiza katika sherehe mbalimbali kubwa za kitaifa kama vile Jamuhuri Day na Madaraka day hadi kwa hafla zinazofanyika hadi ikulu.  Bila shaka hii ni ndoto ya kila msanii kuweza kufikia viwango hivi katika malengo yake ya kimuziki hivyo basi kufanikiwa kwa Ali B katika swala hili lazima kuwe kuna siri fulani anayoitumia..... "usanii sio kuimba tu bali ni hadi vile unavyojiweka kwamba je unaweza ukatumbuiza mbele ya mawaziri au mbele ya rais?kwa sababu usiwe umetobolewa maskio umejichorachora mwili mzima alafu wataka kusimama mbele kumtumbuiza ruto na uhuru,so tusi

Mawaidha Ya Wasanii Mbali Mbali Kwa Kaa La Moto Kuhusu Kupumzika Mziki

Image
Wiki iliyopita kuna habari zlizowashtua wengi saana Baada ya msanii wa hiphop, Kaa La Moto Kiumbe kutangaza kuacha mziki kwa mda. Huu ni uamuzi ambao uliwashtua wengi hadi kumpelekea CEO wa PWANI CELEBRITY AWARDS, Sanita Nzaro kumuandikia barua ya wazi msanii huyo kumsihi msanii huyo kurudi tena kwenye mziki.  Nimechukua mda na kujaribu kutafuta maoni kutoka kwa wasanii waliowahi kufanya kazi na msanii huyu kama vile Susumila, Vivonce, Mswazi Masauti pamoja na Producer ambaye amefanyia kazi zake nyingi Amz Wa Leo ambao kwa pamoja wametoa maoni yao pamoja na kumshauri KAA LA MOTO kuhusiana na uamuzi wake.  Mbali na wasanii hawa aliofanya kazi nao pia Escobar babake ambaye ni msanii aliyewahi kuwa kimya kufikia kiwango cha Kaa La Moto Kumchana katika baadhi ya nyimbo zake kuwa ameshuka kimuziki pia ameweka wazi mtazamo wake kuhusu maamuzi ya KAA LA MOTO pamoja na kumpa ushauri.  Je ni ushauri gani ambao wasanii hawa walimpatia Kaa La Moto ? Escobar alichanwa mara ka

Dazla-Simuigi Diamond, Labda Yeye Ndio Ananiiga Mimi

Image
Msanii hit maker wa track ya KIDE KIDE , Dazla Kiduche amekana madai ambayo yameenea mtaani kuwa anamuigiza Diamond Platinumz . Akiongea katika kipindi cha MwakeMwake cha Pilipili FM na Gates Mgenge, Dazlah ameweka wazi kuwa yeye anajiweka yeye kama yeye na endapo kuna kufanana kwa mitindo na mienendo basi iwe labda Diamond ndio anamuigiza yeye. Dazlah aliyaongea haya wakati akitambulisha kichwa kipya kutoka Tee Hits, Cashhomey ambaye alikua akitambulisha ngoma yake kwa jina Yelele . Kwa sasa Dazlah anajitayarisha kuanza kutayarisha video wiki ijayo ya wimbo wa Kitoriro, kolabo aliyoshirikishwa na mwenzake kutoka Tee Hits, Wynas.