Posts

Showing posts from April, 2016

NEW VIDEO: Queen Renee- GADO / DUMBELELE

Image
Alifanya launch ya kwanza ya video hii ki aina. Lauch hio ilikua ya masaa 36 ambapo alitembelea maeneo tofauti ya burudani na vituo vya redio akiiachia rasmi video hio. Queen Renee ambaye alishawahi wakilisha Kenya katika maonyesho ya Kenya Culture & Fashion Show Nchini Ujerumani ni msanii wa kike anayechipuka kwa bidii sana. Hii hapa ndio video yake  mpya kwa jina Gado / Dumbelele.

Susumila Aongelea Swala la Ajira Na Vijana Wa Pwani Kuhusishwa na Uvivu.

Image
Kulingana na msanii Susumula ni kwamba changamoto za ukosefu wa kazi ziko katika kila upande wa Kenya na sio pwani pekee. Susumila amefunguka na kusema kuwa uvivu uko kila mahali Kenya hii ila kitu kinachofanya mpaka pwani inahusishwa na uvivu ni kwa sababu ni mahali ambapo pako kwenye macho ya wengi tofauti na sehemu zingine za Kenya ..... " ukiangalia barabarani utaona v ijana wamekaa wamevaa jezi za kwamba wanataka kupeana squad kwa matatu tayari ile inaonyesha moyo wa kuwa wanataka kufanya kazi". Kwa upande wa suluhisho la shida hii, msanii huyu ambaye anatarajiwa kuachia video yake na Kaka Sungura wiki ijayo amesema kuwa ni vizuri vijana wazingatie elimu maana unapokua na elimu hata kama huna kazi utakua na ujanja ujanja wa maisha. Susumila ameomba watu wawekeze kwenye talanta za wapendwa wao maana talanta ni moja kati ya ajira kubwa saana Duniani. Bonyeza  HAPA kumskiliza Susumila aka Nugu akifunguka katika mahojiano na Kelvin Jilani(Mtu

Vivonce Awachamba Mabinti Wanaopenda Vya Bure

Image
Msanii wa kike kutoka pwani ya kenya, Vivonce amewapa makavu live mabinti wanaopenda kujianika kwenye mitandao ya kijamii kwa kigezo cha kutafuta njia za mkato kupata mafanikio. Kulingana na Vivonce ni kwamba unapotaka kufanikiwa katika maisha sharti ufanye bidii na ujitahidi vilivyo kutafuta mafanikio kwa njia zinazostahili. Ushauri wa msanii huyu ni kwamba vijana wafanye kazi wakijua wazi kuwa mwanzo wa mafanikio yoyote huwa mgumu ila juhudi na nia humfikisha mtu kwenye mafanikio. "mimi kama the flaglady hua naskia uchungu sana kuona wanawake wenzangu wa Kenya wakijianika katika social media ili wapate wangoso" .... Vivonce amesema katika mahojiano yake na MTUBEI.... Bonyeza  HAPA kuskiliza mahojiano hayo kwa kuna

Nyota Ndogo Aweka Wazi Siri Zinazomfanya Adumu Katika Mziki

Image
Nyota Ndogo ni mmoja kati ya wasanii ambao wamedumu katika mziki kwa kipindi cha mda mrefu na hadi leo bado jamii inamtambua na heshima yake bado iko palepale. Ni msanii ambaye anaweza kukaa kwa mda wa hata wa miaka bila kutoa wimbo na bado anapiga shows za maana. Hivi mbona kuna wasanii wengi wanakuj a wanapotea wanamuacha huyu mwanadada palepale? Hivi mbona wasanii wengi wanatoa hits kila siku ila hawafikii heshima ya Nyota ambaye ni mkongwe na hadi leo heshima yake inazidi kupanda?   Nikimnukuu Nyota , ..."Mimi kama Nyota Ndogo nimetunza heshima yangu kama mama na nimekua kwenye hii industry kwa miaka 16 kwa hivyo ninaweza kupata shows sio kwa sababu niko na kitu kipya hewani bali ni kwa sababu ya heshima yangu na pia niko na nyimbo zinazodumu hewani" .... Haya hapa ni mahojiano ya Nyota Ndogo na Kelvin Jilani( MtuBei ) ambayo nahisi kuwa yana siri nyingi saana za mafanikio na kudumu katika mziki.... Bonyeza  HAPA kuskiliza mahojiano hayo.

SudiBoy Aeleze Kuhusu Studio Yake Na Anayopanga Kuyafanya

Image
Hitmaker wa KuleKule, Sudiboy amefunguka na kusema kuwa studio yake ishakamilika na kilichobaki kwa sasa ni producer ili kazi ianze. Sudiboy pia ameweka vigezo ambavyo ataangalia kwa msanii kufanya kazi katika studio yake. Sudi ameeleza ya kwamba studio yake itahusika n a watu wenye vipaji..... "Kutokee msanii aje afanye kazi nzuri mimi binafsi niko radhi kumsukuma mbele mpaka pale nitakapoweza". Sudiboy amedokeza ya kwamba  Ijumaa hii atakua anaachia wimbo ambao amemshirikisha Brown Mauzo . Mbali na maswala yanayohusu studio yake, Sudiboy amezungumzia matamanio ya Rihaha the boss kufanya kazi naye.... Je amesemaje? Sudi pia amewataja wasanii watu wa kike kutoka pwani anaowakubali . Je wasanii hao ni akina nani? Bonyeza  HAPA kumsikiliza Sudiboy akifunguka kwa kina katika mahojiano yake na Kelvin Jilani (MTU BEI)

NEW MUSIC: Barnaba-WANIFAA

Image
Mkongwe na mkali wa mziki wa bongofleva ambaye anajulikana sana kwa hits za mapenzi na hisia kali ameachia wimbo wake mpya kwa jina WANIFAA. Akiachia wimbo huo, barnaba amesema ya kwamba WANIFAA nunabeba ujumbe ambao unawerza kum,dedicate,ia baba, mama, mtoto, ndugu, rafiki na vilevile mpenzi wako. Ni track kali ambayo imetayarishwa na Producer yuleyule ambaye amekua akitayrarisha hits nyingi za Barnaba na track zingine nyingi, Ema The Boy. Download/Listen   HERE   or  HERE

NEW VIDEO: SautiSol & Mi- Casa – TULALE FOFOFO

Image
Makundi mawili yanayotamba kimziki  mziki hapa Afrika , SAUTISOL kutoka hapa nyumbani Kenya na MI CASA kutoka Afrika Kusini wameangusha video mpya wa wimbo TULALE FOFOFO.

NEW MUSIC: Nuh Mziwanda Feat AliKiba - JIKE SHUPA

Image
Aliyekua akim,date Shilole na kusemekana kwamba alikua akipokea kipigo kutoka kwa mpenzi wake Nuh Mziwanda , hitmaker wa track kama vile Bilima baada ya kukaa kimya kwa kiasi cha haja amevunja ukimya wake kwa kuachia hit hiii aliyomshirikisha star wa bongfleva, AliKiba . Ni track ambayo imetayarishwa na Prodcuer Mr. T Touch. DOWNLOAD/LISTEN  HERE or HERE  

Tamasha Kubwa Afrika Mashariki Kufanywa Mombasa Wikendi Hii

Image
Mwishoni mwa mwezi huu, Siku ya Jumamosi 30 Aprili, Mombasa itakua mwenyeji wa takriban wamama 100,000 kutoka sehemu mbalimbali hapa afrika mashariki. Wanawake hao watakua wanahudhuria uzinduzi rasmi wa mradi wa AMSHA MAMA.  AMSHA MAMA ni mradi wa kuwasaidi ake na mama kujiendeleza na kuwapa uwezo wa kujitegemea kibiashara na kujiinua kimaisha. Mradi huo unaendeshwa na Joe Kariuki ambae alikua mmiliki wa recording label ya CANDY N CANDY na ambaye hivi majuzi aliorodheshwa kua mwamfrika nambari mbili mwenye maono makubwa, katika orodha ambayo aliwashinda wangwiji kama vile bilionea Aliko Dangote .  Katika uzinduzi huo, kutakua na maonyesho ya biashara mbalimbali kutoka kwa wamama kutoka pande zote za afrika mashariki, wakiuza na kuonyesha baadhi ya biashara na bidhaa zinazowaendesha maisha yao. Tamasha hio kubwa ya uzinduzi wa AMSHA MAMA utafanyika katika uwanja wa mama ngina na kutakua na burudani la kukata na shoka kwani kutakuwepo na Susumila, Sudiboy, Nyota Ndog

NEW MUSIC: Queen Renee - GADO(DUMBELELE)

Image
Ni mmoja kati ya wasanii wanaochipuka na ana bidii sana na kazi yake. Mwezi jana tu ndio aliachia wimbo na video yake mpya na sasa ameachia mzigo mpya tena  kwa jina GADO / DUMBELELE . Wimbo ambao anaimbia mpenzi wake akieleza jinsi anavyompenda na alivyo na nthamani kwake.... DOWNLOAD / LISTEN HERE

NEW MUSIC: Mafikizolo Ft. Diamond Platinumz & DJ Maphorisa - COLORS OF AFRICA

Image
Ni collabo ambayo ilikua ikingojewa sana toka mwaka jana. wasauzi hawa, hit makers waa Kona wakiwa wamemshirika msanii anayetamba sana kwa sasa Afrika Mashariki, Diamond Platinumz na DJ Maphorisa. DOWNLOAD / LISTEN HERE  

Papa Wemba Afariki Dunia (video alivyoanguka jukwaani)

Image
Mwanamziki mkongwe wa nyimbo za lingala mwenye mika 66, Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba au Papa Wemba kama anavyojulikana amefariki dunia. Papa Wemba alianguka jukwaani akitumbuiza katika tamasha la tisa la FEMUA ( FEMUA 9 ) katika mji wa Abidjan, Ivory Coast . Papa walidondoka stejini na kuanguka wakati wanenguaji wake wakiendelea kutumbuiza bila kujua yaliyokua yamejiri. Wahudumu wa shirika la RecCross walikimbia kumsaidia pamoja na wanabendi wake lakini wakapata ugumu wa kumuamsha na kumrudisha katika hali ya kawaida, jambo ambalo liliwafanya wamkimbize hospitalini. Punde tu baada ya tukio hilo, manager wake alipost na kifaransa katika ukurasa wake wa Facebook, nikitafsiri: “I do not have the strength to put this information on Facebook,...Papa Wemba fell on stage at Anoumabo, Abidjan where he was performing at the Legislative Femua festival, organized by the Magic System. There’s more scared than hurt. As a manager, I assure you on his state of health and beg yo

Mercy Masika Ahusika Katika Ajali Ya Barabarani

Image
Mwanamziki wa Injili ambaye wimbo wake wa MWEMA ulihit sana na bado unaendelea ku,enjoy airplay kubwa amenusurika kifo katika ajili ya barabarani usiku wa Jumamosi 23, April kuamkia Jumapili 21, April. Mercy amenusurika ajali hio bila hata kukwaruzika popote. Ajali hio ambayo ilihusisha gari lake ambyo iligongwa kwa nyuma na trailer ilitokea katika barabara kuu ya Thika SuperHighway . Japo awali kulikua na uvumi ya kwamba Mercy alikua hali mahututi akipigania uhai wake katika hospitali ya Aga Khan, Mercy ameweza kuweka wazi ya kwako ako salama salmin. Kupitia handle yake ya Twitter, Mercy ambaye ameolewa na David Muguro kwa takriban miaka saba sasa na wamejaaliwa watoto wawili ( Ranise Mugur o na Tevita Muguro ) amepost: “I take this time to say am (sic) completely out of danger and without even a scratch from the accident. I serve a living God,”

Rihaha The Boss Ataja Msanii Anayetamani sana Am,Manage

Image
''Rihaha the boss'' ambaye kwa sasa ameandikisha mafanikio makubwa saana katika kazi yake ya kuwasimamia wasanii amefunguka na kusema kuwa baadhi ya sifa ambazo msanii anafaa kuwa nazo ndio a,fit katika management yake ni bidii na nidhamu . Aliongezea kuwa, lazma msanii mwenyewe awe na malengo ya kutoka hatua moja hadi nyingine.  Zilikuwepo fununu kuwa Rihaha alikua na mpango wa kuwasimamia Shaa Bigg y na Dogo Richie ila mpango mzima ukafeli. Je kulitokea nini na chanzo cha mpango huo kufeli ni nini? Je unajua kwamba kuna msanii kutoka mombasa ambaye Rihaha ametamani saana kumsimamia,ungependa kumjua?... Msikilize Rihaha akitiririka katika mahojiano yake na Kelvin Jilani/MTU BEI HAPA

Dalili Za Collabo Ya Nyota Ndogo, Ali B Na Susumila

Image
Ndio vigogo wa mziki wa kizazi kipya hapa Pwani. Wamekua wakikonga nyoyo za wengi kwa tungo zao kwa mda wa miaka mingi sana. Wamekua wakiipeperusha bendera ya ZIKI LA NAZI , si Kenya tu bali Afrika Mashariki na dunia nzima kwa ujumla. Kabla ya Nyota Ndogo kusafiri kuenda Tour nchini Denmark alikua anafanya projects zake Tempoz Records kwa producer AMZ . Tempoz pia ndio studio ambayo Susumila amekua akifanyia nyimbo zake nyingi katika siku za hivi karibuni. Na pia Ali B kazi yake ya mwisho, BEMBEA aliifanyia Tempoz na kunazo ambazo ziko jikoni anazifanyia Tempoz bado. Watatu hawa wamejuana kwa mda mrefu kwani wamewahi kufanya kazi nyingi kwa pamoja kama vile roadshows, clubshows na hata show za kampeni za siasa ila katika hivi siku za karibuni wamekua na ukaribu sana kwani mara nyingi wamekua wakionekana pamoja katika mikahawa, tamashani na hata studio..haswaa TEMPOZ . Kwa kua wamekua wakipatana mara nyingi Tempoz, inakisiwa ya kwamba watatu hawa wanatayarisha

Susumila Na Producer Amz Wafanya Sherehe Ya Kumkaribisha Nyota Ndogo

Image
Alitoka nchini mwishoni mwa mwezi wa Januari akielekea Denmark ambako alikua amealikwa katika sherehe ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya legendari wa mziki wa reggae marehemu BOB MARLEY. Kando na sherehe hio, Nyota alikua alikua atakita kambi kwa miezi miwili na usu nchini Denmark ambako alikua anafanya tour na kufanya collabo za wasanii wakimataifa. Baada ya kukamilisha tour yake wiki jana, alirudi nyumbani na akafanya show Skylounge, show ambayo ilijaaa sana na kuhudhuriwa na watu wengi maaruf na mashabiki wengi sana. Hapo jana, siku ya Jumatatu, Susumila na Producer Amz waliandaa sherehe ya kumkaribisha rasmi Nyota Ndogo . Sherehe hio ambayo iliitwa PWEZA PARTY iliweza kuhudhuriwa na familia ya Nyota Ndogo, wasanii kama vile Ali B, Pero, CashEra, Hustla Jay, Vivonce, Wazo Baba, Res T, Gaspery, Msanii Jrg na wenginene wengi. marafiki na washika dau wengine katika tasnia ya burudani kama vile mtangazaji Lukas De Mackinon wa FM, Producer Jay Crack, Hassan Faisal, Kibibi

Wasojali Band Kufanya Collabo Na Yamoto Band

Image
 Ni vijana wanne ambao wa sasa wamatesa sana na video ya wimbo wao wa NITALIA NAWE ambao walishirikiana na Kelechi Africana ambaye wamesajiliwa wote katika Kubwa Entertainment inayomilikiwa na Athman Babaz . Katika siku za hivi karibuni, wamekua katika jiji la Nairobi kufanya media tour kuskuma video yao na mziki wao kwa ujumla. Na safari hio haikua bure kwani inaonekana imezaaa matunda hata zaidi ya waliyokua wanatarajia au wamepanga kutimiza. Nasema hivyo kwa kua kwa sasa Wasojali Band wako katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kufanikisha collabo yao na Yamoto Band kutoka Tanzania. Kupitia njia ya simu, nikiongea na meneja wao, Athman Babaz , alieleza ya kwamba bado vitu kidogo tu wakamilishe ili makubaliano hayo yaishe lakini kufikia sasa yale mazungumzo yalipofikia haoni kama kuna kitu kitazuia collabo hio. Athman alizidi kueleza ya kwamba mazungumzo yatakapo kamilika tu wataenda nchini Tanzania kwa madhumuni ya kurekodi na kuandaa video ya collabo hio.

NEW MUSIC: Gaspery Feat Kaa La Moto - NIAMBIE NIJUE

Image
Gaspery Mwakatengo ambaye jina lake la kisanii ni Gaspery ni msanii ambaye anachipuka na kwa kasi sana. Ni msanii ambaye ana bidii na anajaribu sana kufanya vitu tufauti chini ya management ya Vidudu Classic. Alifanya track ya kwanza- SHANGINGI, Mwaka jana, 2015 ambayo alimshirikisha Kigoto chini ya Producer TK2.  Kwa mara ya pili, amekuja na Kaa La Moto chini ya mikono ya Producer AMZ. '' Oyoo Kaa La Moto Hivi ni hit song ama ni connection...  ama ni kuhonga kwenye hizo radio station.... mbona we unachezwa ama unakula nao... ama kisa niukali ndo Unakaa kwa chati zao....'' Hio ni kati ya mistari iliyopo katika pini hili jipya... hivi ni nini watakua wameongelea? Pakua uskilize DOWNLOAD / LISTEN HERE    

Flavour Atatiza Mitandaoni Na Picha Hii Ya Uchi

Image
Kuna mambo ambayo  hufanyika sana katika showbiz, ila mengi yanapenda sana kufanywa na wasanii au celebrities wa ughaibuni na iwapo ikitokea Afrika basi hua inakua issue sana kwa sababu mila, desturi na tamaduni za Afrika haziruhusu. Mara nyingi wau waarufu ulaya haswaa wa kike wamekua wakijipa kiki kwa kupiga picha za nusu uchi au uchi kabisaa na kuweka mitandaoni. Msanii kutoka Nigeria, Chinedu Okoli aka Mr Flavour naye ameamua kwamba ataenda na mkondo huo kwanikatika account yake ya Instagram   alipost picha ambayo inaonekana ako uchi ila ameficha sehemu nyeti zake na guitar tu. Wapo walioona ni sawa na wapo waliona ya kwamba Flavour amechemkaa, mfano kuna shabiki aliyesema ya kwamba wanaume wa kweli wanapost picha za watoto wao, wapenzi wao na marafiki ila si picha ya kilimbukeni kama hio.

Mr Blue Afunga Ndoa

Image
Kheri Sameer Rajabu aka Mr Blue alifunga ndoa hapo jana. Mr Blue alifunga ndoa na Waheeda ambaye ndio amam wa watoto wake wawili. Sherehe hio ambaye ilifanywa kimya kimya sana ilihudhuriwa na watu wa wachache sana ambao wapo karibu na wanandoa hao.

Jovial Afunguka Na Kueleza Jinsi Wasanii Hujitakia Wenyewe Kutumiwa

Image
Msanii wa muziki kutoka Mombasa , Jovial amepuuzilia mbali dhana ya kuwa fursa za kimuziki ziko Nairobi pekee. Kulingana na Jovial ni kwamba, fursa ziko mahali popote pa le kinachohitajika ni bidii ya msanii katika kuskuma mziki wake na kutafta connections.  "ukiwa na akili na unajua ku hype kazi yako na unajua kuzungusha kazi zako yaani opportunites ziko kila mahali sio Nairobi sio Mombasa inategemea na bidii yako". Jovial ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake cha Unakosa Raha pia aliongeza kuwa wasanii wengi wanafeli wakienda Nairobi kwa sababu wakipata deal yakufanya kazi na studio kubwa za Nairobi wanazidiwa na furaha kiwango cha kutozingatia mikataba. "Mtu anapata deal anakua confused to an extent hafikirii kama kuna kusign hafikirii hivyo vitu vidogo vidogo believe me they pay because ukifanya kazi na msanii mkubwa and u dont notice those little things utakua umefanya mziki na yeye yeye anapokea wewe hupokei coz huezi claim ile song unak