Posts

Showing posts from July, 2016

NEW TRACK:CML-BAO NISHAFUNGA

Image
CML aka SWENG BOSS ni msanii wa hiphop ambaye kwa sasa amekita kambi Tempoz, chini ya uangalizi wa Producer Amz. Ni msanii ambaye ukimskia akirap utajua wazi ana uwezo mkubwa ndani yake na ni mda mchache tu ataanza kupelekana bega kwa bega na wanahiphop wengine waliobobea. BAO NISHAFUNGA ndio track yake mbichi kabisa. Track ambayo imetayarishwa na Producer Amz... ipate HAPA

Je Wamjua ELPARAISO?

Image
Neno ‘Elparaiso’   ni neon la kitaliano linalomaanisha pepo/paradise …   Ila hapa tunaongelea kuhusu model ambaye hafanyi kazi zake   hapa nchini tu ila pia amekua akisafiri katika nchi mbali mbali. Japo hajafikisha hata miaka 25, ‘Elparaiso’ anasema kwamba ana tofauti na wasichana na models wengi ambao hua wanaishi kutegemea ‘sponsors’   kwani yeye anakula na jasho lake. Model huyu ambaye yuko kwenye mahusiano anasema anafurahi kwa kua na mtu anayemuelewa kazi yake kwani kusafiri kwake mara kwa mara ni changamoto. ‘kusema kweli kua ‘Elparaiso’ si rahisi ila mziki hunifariji sanasana nyimbo za Alikiba . Napenda sana kuangalia na kufuatilia sana na nashabikia Arsenal . Unaweza kujua mengi zaidi kumhusu kupitia: Twitter: Elparaiso Instagram :   Elparaiso Facebook: Luciel Parasio Snapchat: Elparaiso

Bizzy Kay Aanzisha Kampuni Ya Ku,manage Wasanii

Image
KIMWANA, track ambayo aliwashirikisha   Ali B na Susumila ni moja kati ya track zake mbazo zimewahi kupendwa sana na mashabiki. Bizzy K ambaye ana uwezo mkubwa sana wa utunzi na kuimba katika siku za hivi karibuni ameonekana kupunguza kasi yake ya mziki. ‘kwa sasa kidogo nimepunguza kazi zangu za mziki, ila hivi karibuni naachia ngoma mpya. Kando na usanii mimi ni mwanabiashara na sanasana nimeekeza katika ‘real estate’ hivyo basi katika kufuatilia fuatilia hii mijengo yangu hua nashikika sana hadi nakosa mda wa kufanya mziki. Lakini napenda mziki sana na mziki ni biashara ambayo mtu akiifanya kwa ustadi itampa faida kubwa sana so nimeamua sasa nianze ku,manage wasanii. Japo sitakua nawasimamia mimi mwenyewe moja kwa moja kwasababu nitakua na manager na watu wengine watakaokua wanashuhulikia maswala hayo, mimi ndiye nitakaye kua nasukuma mchakato mazima wa management hio’ Bizzy Kay amesema. Akifafanua zaidi Bizzy K amesema ya kwamba bado hajachagua wasanii amb

Akatazwa Kuachia Wimbo Na Mpenzi Wake

Image
Ni msanii ambaye ana potential ya kuja kua msanii mkubwa sana wa hophop kutoka Pwani . Flamez ambaye alikua amejipanga kuachia track yake mpya ya PENZI LA ATM aliyomshirikisha Shaa Biggy imebidi asitishe project hio kisa   mapenzi. Kilichoimbwa katika wimbo huo ndio sababu kubwa iliyofanya kutokea kwa mtafaruku huo wa kusababisha track hio kufikia kusitishwa. Katika track hio, Flamez anasuta mabinti ambayo wameendekeza pesa mbele katika mapenzi na mpenzi wake akaichukulia akaona ya kwamba ujumbe huo umemlenga yeye. ‘ Si kweli kwamba nimelenga track hio kwa mpenzi wangu ila nilikua nimeongelea uhalisia wa vitu vinavyotokea ila sasa yeye kaichukulia personal hadi kusema ya kwamba atajitoa katika mahusiano yetu iwapo nitaachia track hio kwa kua anadhani ntakua namdhalilisha. ’ Flamez amesema. Flamez ambaye vilevile alikua ashaanza mikakati ya kuaanda video ya track hio imembidi arudi kwenye ‘drawingboard’   huku akisema ya kwamba inamuuma sana ila hio baadhi ya cha

Watu Wananielewa Vibaya.. Dazlah Aeleza

Image
Star wa Kidekide , Dazlah Kiduche alishambulia mishale ya lawama na hata matusi kutoka kwa mashabiki wake hapo jana baada ya yeye kuweka picha ya poster tatanishi ya track mpya aliyofanya na Sis P. Kulingana na tukio zima kilichowaudhi mashabiki wake n i uamuzi wa wasanii hao wawili kuweka nguo ya ndani ya mwanamke katika poster hiyo jambo ambalo halikukera tu mashabiki wake bali hadi wasanii wenzake pamoja na wadau wakubwa wa sanaa. Wengi wanahisi kuwa Poster hio iko nje na maadili pamoja na kumdhalilisha mwanamke. Je Dazlah analizungumziaje sala zima? Bonyeza  HAPA kumsikiliza

Naishi Maisha Yangu, Sitafuti Kiki. Sis P Aeleza

Image
Msanii Kutoka hapa Pwani , Sis P amesema kuwa haifai kamwe watu kumhukumu na ni jinsi gani anaishi maisha yake. Kulingana na Sis P ni kwamba mbali na yeye kuwa msanii yeye pia ni binadamu kama watu wengine...... "mimi sio mtu wa kujidanganya,..ido what i feel like doing,..am not just limited to certain things if u become too serious people will get bored" ..... Sis P Queen ni mmoja kati ya wasanii ambao kwa kipindi cha mda mrefu amekuwa akiandamwa na scandal baada ya scandal ikiwemo ya yeye kuwa na uhusiano na maproducer. Sis P Queen amefunguka mengi alipokua akifanya mahojiano na MtuBei. Sis P ameongea mengi kwa kina   kuhusu mahusiano yake na project yake na Dazlah. Msikilize   HAPA

Rawbeena Aachia Video iliyomgharimu Nusu Milioni (NIPOZE)

Image
Ni mmoja kati ya wasanii wanaokuja kwa kazi na anajitolea sana kufanya kazi kwa video. Anajiita hustler kwa kua ni mtaftaji sana. Mwanzoni mwa mwezi huu, manager alidokeza ya kwamba  walikua wamemaliza kutayarisha video ambayo ilikua imewagharimu Kshs. 500,000. 'Tumeamua kufanya video ya gharama kubwa kwa kua tunataka kazi yenye kiwacho cha mataifa si video ya kubahatisha' manager alinieleza. Video hio ambayo inatarajiwa kuteka anga za mziki imeandaliwa na  Rikky Bekko wa BigDreams Media.  

Picha Za Utayarishaji Wa Video Ya SUSUMILA na AVRIL **EXCLUSIVE**

Image
Kwa mda wa takriban mwezi mmoja hitmaker wa OYOO amekua akitangaza mwanzo wake mpya ambao atakua anaachia video na audio mpya na vilevile label mpya. Amekua akisema ya kwamba amemshirikisha msanii flani wa kike kutoka Nairobi ila amekua akibana jina. Hatimaye hapo jana aliweka wazi kupitia ukurasa wake wa facebook ya kwamba  kazi anayoiachia karibuni atakua memshirikisha Avril . Washa,shoot video hio na director Rikky Bekko wa BigDreams Media na hizi ni picha walipokua wanaanda video hio. Picha kwa hisani ya EXPLODE AFRICA ( 0706013617)

Wasanii Kutoka Likoni Wapewa kshs.500,000

Image
Hapo jana   siku ya jumapili, 24-Julai Muwakilishi wa Wanawake wa kaunti ya Mombasa, Mishi Mboko aliweza kukabidhi wasanii kutoka Likoni, Talent House   hundi ya Kshs. 500,000. Hundi hio ilitolewa wakati mheshimiwa Mishi Mboko alipokua akikabidhi mitaji/capital kwa makundi mbalimbali kutoka eneo la Likoni ili waanzishe mirandi itakayowapa uwezo wa kujitegemea na kujiendeleza kimaisha. Fisherman ambao ni mmoja wa waanzilishi wa kundi hilo la wasanii, Talent House kutoka Likoni ameeleza ya kwamba hundi hio wameweza kukabidhiwa baada ya kuandika proposal takriban miezi mitano iliyopita na kuiwasilishwa katika ofisi za muwakilishi wa wanawake wa kaunti ya Mombasa. ‘…Haikua mara yetu ya kwanza kuwasilisha proposal kwani tuliwahi kuwasilishwa proposal katika afisi ya mbunge wa Likoni, mheshimwa Mwahima na afisi mbalimbali lakini hazikuwahi kupitishwa. Ni vigumu kupata usaidi haswa kifedha kutoka kwa waheshimiwa unless uwe na proposal lakini bila hivyo hawawezi kukup

Waathiriwa Wa Baa La Njaa Ganze Waanza Kupokea Msaada (picha)

Image
Wiki jana eneo la Jila, Bamba katika kaunti ya Kilifi liligonga vichwa vya habari   baada ya kuangaziwa jinsi watu wanavyoteseka na njaa.   Zilikua habari za kushtusha na kuhuzunisha kwani watoto wanailisemekana kwamba wapo ambao wamepoteza maisha kwa kukosa chakula madai ambayo serikali imeyakana kwa kusema ni kweli kwamba watu wanatesekan na njaa ila hakuna aliyepoteza uhai. Habari hizo ziligusa wengi na kati ya walioguswa na habari hizo ni Hasheem Omar   (Rihaha ) ambaye anatokea kunti hio ya Kilif i. Alimuomba director, Kalpesh Patel wa kampuni anayoifanyia kazi ( Export Trading Co. Ltd) aingilie kati na kupitia kampuni hio wakapanga kuenda kusaidia wa balaa la njaa huko Bamba. Wakiwa na dozen 100 za vitabu, mbaazi tonne 10, maharagwe tani 6, unga wa mahindi tani 20, biskuti catoni 100 na peremende katoni 8 …ikiwa ni mzigo wa takriban Shilingi Milioni Mbili walifunga safari hapo siku ya jumamosi kutoka Mombasa hadi Kilifi ambapo waliambatana na county Co