Posts

Kwa Sasa Inapatikana Kwa www.machampalimedia.com

Image
Usipitwe na habari, matukio na vitu vingine vingi vipya vinapochipuka.Utaendelea kupata uhondo wote uliokua ukiupata humu ndani kupitia www.machampalimedia.com . Ni bora zaidi na vitengo vingi zaidi, usipitwe, bonyeza  >>  HAPA << uweze kuji,update.

Mashabiki Wawaweka Roho Juu Dizzle Na Dogo Richie

Image
Baada ya kufanya vizuri kwa wimbo KIFAA, ambao Dizzle alimshirikisha hitmaker wa Mziki Majanga , hatimaye wawili hao wameachia video hio ambayo ilikua imesubiriwa kwa hamu na gamu. Kulingana na wawili hao ni kwamba hawakua na nia ya kufanyia video wimbo huo lakini mashabiki ndio waliowaskuma kufanya hivyo. 'Baada ya kuachia KIFAA tu, nilikua nikiulizwa kila siku kama nitaachia lini video yake. Nikapuuza mwanzoni lakini mskumo kutoka kwa mashabiki ulizidi kwani idai ya wanaouliza swali hilo ikawa inaongezeka nikaona sina budi ila kuwapa wanachotaka kwa sababu mwisho wa siku huu mziki nafanyia mashabiki, na nafaa kuwapatia wanachohitaji .' Alielezea Dizzle wakati akitambulisha rasmi video hio iliyoongozwa na Ricky Bekko wa BigDreams . Itazame hapa...

Hiki Ndicho Alichokifanya Baada Ya Kutimuliwa Studio

Image
Angekua na moyo mwepesi basi hata tusingewahi kumsika kwani   kilichomtokea katika jaribio lake la kwanza kufanya mziki kingemkatisha tama ila kwa kua alikua na malengo ya juu hakutetereka ila aliogeza ujasiri na moyo zaidi wa kufikia malengo yake. Adily Tozy alianze kupenda mziki tangia akiwa mtoto. Miaka miwili iliyopita Adily ndipo alipoona ya kwamba wakati mwafaka wa kuanza mziki rasmi umewadia. Akajizoazoa akiwa amejihami na mashairi kuenda studio afanye mawili matatu. Baada ya kupitishwa huku na kule kwa mda kiasi hatimaye alionana na   producer ambaye alimuandalia beat ya wimbo na kumpa akajitayarishe kurekodi. Alirudi studio baada ya wiki mbili na akabaahatika kupata mda mzuri na producer wake. Baada ya kuwa studio kwa zaidi ya takrriban masaa mawili wakijaribu kuandaa wiimbo wake wa kwanza, producer aliona ya kwamba msanii huyo likua hawezi kabisa na akaamua kumtoa nje ya studio na kumrudishia pesa zake na kumwambia   asiwahi kurudi tena katika studio hio na us

Susumila Alilia Mapenzi Mwezi Mmoja Kabla Kufunga Ndoa Tena (Video)

Image
Ikiwa bado mwezi mmoja tu kabla msanii Susumila kuuasi ukapera, amekutana na Timmy T Dat ambaye kwa pamoja wamefanya bongea la video la wimbo OYOO (Nipende) ambapo wanaonekana kulilia  mapenzi. Ni video iliyoandaliwa na Ricky Bekko wa BigDreams. Itazame hit hio mpya hapa chini...

Susumila Amshirikisha Timmy T Dat kwa Hii Mpya

Image
Katika siku za hivi karibuni, katika hatua ya kujiongezea mashabiki haswaa katika jiji la Nairobi na Kenya nzima kwa ujumla, msanii Susumila amekua akifanya collabo na wasanii tajika kutoka jiji la Nairobi. Alianza na MAPEPE ambayo kulingana na yeye, hio ndio ilikua track yake iliyofanya vizuri zaidi mwaka wa 2016 alafu baadae akafanya WEWE aliomshirikisha Avril, wimbo ambao video yake ndio video ya Susumila ambayo imefanya vizuri zaidi katika mtandao wa Youtube.  Ukiwa ni mwaka mpya sasa, msanii huyu ambaye anatarajiwa kufunga pingu za maisha mwezi wa Aprili, amemshiriikisha Timmy T Dat ambaye kwa sasa ndiye msanii anayepeta zaidi nchini Kenya. Ni wimbo ambao ulitayarishwa na Producer Totti. Kupata kuskiziliza na kupakua hit hio, bonyez>>  HAPA

Kijana Wa Miaka 26 Aeleza Alivyomzidi Naibu Gavana Wa Kaunti Ya Mombasa

Image
Joto la siasa linapamba moto wakati huu tunapokaribia uchaguzi. Hivi sasa wanasiasa wengi wapo mbioni kujipigia debe wakijiandaa kuenda katika mchujo ili wapate tiketi ya chama ambacho watakua nacho kwenye debe ifikapo Agosti 8. Katika chama cha Jubilee ,   ni wagombea wawili tu ambao watakua wanapigani tikiti   ya chama hicho kuwania nyadhifa ya useneta wa kaunti ya Mombasa, naibu wa gavana wa kaunti ya Mombasa, bi Hazel Katana na bwana Abuubakar   Swabir .   Abuubakar ambaye anajipigia   upato kumpiku bi Hazel , amesema ya kwamba kuna vigezo vitano ambavyo vinampa   ujasiri wa yeye kumuangusha bi Hazel . ‘Huu ni wakati wa mageuzi, wananchi wamechoka na uongozi uliopo ndio maana watu wanataka watu wapya kabisa na ukiangalia mpinzani wangu, yeye si mgeni wa siasa kwa hivyo sioni kama ataweza kuwa kipenzi cha wengi kwa hilo….’ ‘Isitoshe, mwenzangu amekua katika serikali ya kaunti tangu kuanza kwa mfumo wa ugatuzi. Kwa miaka yote minne hio, hakuna maendeleo aliyofany

Cannibal Azungumzia Video Inayomuonyesha Akiwa Mlevi Chakari

Image
Siku ya Jumapili msanii Ralph Masai almaaruf Cannibal ambaye anagombania nyadhfa ya MCA Mtopanga ward alikua gumzo mitandaoni baada ya kuzaa kwa video iliyomuonyesha amelewa chakara. Ni video ambaye ilimfanya akashifiwe kwa sana. Wengi wakisema ya kwamba amejidhalilisha na amekosea kufanya kitendo kama hicho haswa ukizingatia ya kwamba anataka kua kiongozi , si wa vijana tu bali jamii nzima. Hatimaye Cannibal amefunguka na kuongea kuhusu kipande cha video hicho…  ‘Ukiskia ya kwamba siasa ni mchezo mchafu usidhani ni msemo tu. Ile video ni mimi ukweli, ila ni ya miaka sita nyuma, kitambo sana hata mimi ilinishtua kuipata mtandaoni siku ile. Tulifanya uchunguzi na kujua ya kwamba watu waliohusika kusambaza video ile ni wapinzani wangu ambao wanagombani nyadhfa ninayogombania pia.’ Cannibal amesema na kuongezea ya kwamba wapinzani wake wameingia mashinani na kujua ya kwamba yeye ndio kipenzi cha watu na hawana nafasi ya kumpiku ndio maana wakaamua kutumia njia chafu ili kumchaf