Joto la siasa linapamba moto wakati huu tunapokaribia uchaguzi. Hivi sasa wanasiasa wengi wapo mbioni kujipigia debe wakijiandaa kuenda katika mchujo ili wapate tiketi ya chama ambacho watakua nacho kwenye debe ifikapo Agosti 8. Katika chama cha Jubilee , ni wagombea wawili tu ambao watakua wanapigani tikiti ya chama hicho kuwania nyadhifa ya useneta wa kaunti ya Mombasa, naibu wa gavana wa kaunti ya Mombasa, bi Hazel Katana na bwana Abuubakar Swabir . Abuubakar ambaye anajipigia upato kumpiku bi Hazel , amesema ya kwamba kuna vigezo vitano ambavyo vinampa ujasiri wa yeye kumuangusha bi Hazel . ‘Huu ni wakati wa mageuzi, wananchi wamechoka na uongozi uliopo ndio maana watu wanataka watu wapya kabisa na ukiangalia mpinzani wangu, yeye si mgeni wa siasa kwa hivyo sioni kama ataweza kuwa kipenzi cha wengi kwa hilo….’ ‘Isitoshe, mwenzangu amekua katika serikali ya kaunti tangu kuanza kwa mfumo wa ugatuzi. Kwa miaka yote minne hio, hakuna maendeleo aliyofany