Posts

Showing posts from March, 2016

NEW MUSIC: Yamoto Band- NIGANDE

Image
Moja kati ya makundi yanayotesa sana Afrika Mashariki. Wanapeta sana anga za mziki na hua wako,booked sana hata kuwapata kwa show ni balaa. Huu hapa ni mdundo wao mpya, kama kawaida, hawachezi mbali na mapenzi. DOWNLOAD / LISTEN HERE or  HERE

NEW VIDEO: Eddy Ticha - ZAWADI

Image
Ni mmoja kati ya wasanii ambao wana uwezo mkubwa sana wa utunzi na sauti. Huyu jamaa alishawahi fanya album nzima bila kutoa video lakini ameamua ya kwamba huu ni mwaka mpya wa kufanya vitu vipya ndio maana project yake ya kwanza mwaka huu imefuatiliwa na video yake hii. Ni wimbo uliotayarishwa na Morbiz Sheriff, Thurnder, Sound Records na video imeongozwa na Lynke Jr, Damusik Lab.

NEW VIDEO: Queen Renee- SWEET LOVE

Image
Queen Renee , ambaye alizindua album yake ya Kamata Champagne na pia kutambulisha track yake ya pili kutoka kwa album hio ameachia video ya track hio kwa jina SWEET LOVE . Ni video ambayo itakua inatambulishwa rasmi leo Dans Lounge, Valencia Inn katika katika #CelebrityThursday.  

NEW MUSIC: Serah Sarah -UKIRUDI

Image
Kama ni sauti basi huyu dada kabarikiwa, na tungo zake hapa ameonyesha umahiri. Baada ya kuhit na Cheza Kidogo, Serah Sarah amerudi tena kukonga nyoyo zetu na UKIRUDI , Track ambayo imeandaliwa na Producer Mastola ambaye ni MCongo. Umbali aliopo na nyumbani hauja uruhusu uwe kikwazo katika kutengeneza mziki ambao soko lake kubwa ni Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla kwani katika kutayarisha wimbo huu ilim,bidi kumsafirisha Producer Mastola hadi Dubai aliko ili kumtayarishia wimbo huu, kama vilevile alivyomgharamia Hamza Omar, ONE MONTAGE FILMZ kuenda kumfanyia video ya wimbo huu. Bonyeza  HAPA au  HAPA kuusikiliza/pakua

NEW VIDEO: Serah Sarah -UKIRUDI

Image
Baada ya kuhit na Cheza Kidogo ambayo alikua amemshirikisha Dazlah, hitmaker wa Kidekide, Serah Sarah ameachia bonge la video....bonge la video yani. Ni video ya track yake mpya kwa jina UKIRUDI . Hamza Omar wa ONE MONTAGE Filmz ndiye aliyetayarisha video hii ambayo iliandaliwa Dubai.

Susumila Afunguka Kuhusu Pete Zake na Uhusiano Wake na Gavana Joho Baada ya Kampeni za Malindi

Image
Hii leo katika Kipindi cha MwakeMwake , kinachoendeshwa na Gates Mgenge, Pilipili Fm , kuanzia saa tisa jioni hadi saa moja usiku Susumila amefunguka ya kwamba ana jumla ya pete kumi na tano na kati ya pete hizo, ile ambayo ina thamani zaidi ni ya gharama ya ....   Je pete zote hizi ni za nini? Kwa mda mrefu saana sintofahamu imegubika kitendo cha msanii Susumila kumiliki na kuvaa pete kibao sana mikononi mwake huku baadhi ya watu wakifikia kiwango hata cha kuhusisha pete hizo na nguvu za giza. Kwa mara nyingine Gates ametaka kufafanuliwa zaidi umuhimu wa pete hizi kwa maisha ya Susumila. Nikimnukuu Gates .."labda pete zako huwa wazitumia na nini, ni mapambo au maanake one time Chapatizo alisema kwamba hapa Mombasa na huu mziki hauwezi fanya bila kujikinga".. swali hili Susumila akalijibu, nikimnukuu "kila mtu huwa anafanya vitu apendavyo yeye mwenyewe, kuna mwingine anafuga rasta kwa sababu ya dini yake, wengine wanafuga rasta kwa kuwa ni fashion, umenielew

Kionjo Cha Video Ya Sera Sarah - "UKIRUDI" Itakayodondoka Leo

Image
Mwaka jana aliachia bonge la project, Cheza Kidogo . Track ambayo iliweza kuteka anga za mziki kwa fujo. Akimshirikisha  Dazlah ambaye alikua anapeta na KideKide, track hio iliweza kuteuliwa katika kitengo cha Best Collaboration Of The Year na pia katika kitengo cha Video Of The Year japo kua haikuweza kushinda katika vitengo vyote viwili katika tuzo za Pwani Celebrity Awards. Na sasa Serah Sarah anadondosha UKIRUDI . Ikifika Mida ya saa kumi hivi, video hio ambayo imeongozwa na kutayarishwa na Hamza Omar wa One Montage Films. ITAZAME HAPA  

NEW MUSIC: Queen Renee- SWEET LOVE

Image
Alirudi wiki mbili zilizopita kutoka Ujerumani ambako alikua ameitikia mwito wa mwaliko katika Kenya Culture & Fashion Show. Akirudi alisema ya kwamba anajipanga kuanza media tour, na kabla kuanza media tour ambayo atakua ana,promote Album yake ya Kamata Champaign , ameachia Sweet Love ambayo ni track yake ya pili katika album hio. DOWNLOAD / LISTEN HERE or HERE

NEW MUSIC: GZee Feat Shaa Biggy- KaaZeze

Image
Msanii mkali kutoka kuleee Kilifonia , GZee amemshirikisha Shaa Biggy katika KaaZez e. Ni version ingine ya track ambayo walikua wameifanya kitambo wakaiita Hisi Kali . Audio ndio hii imetangulia na video ipo jikoni katika hatua za mwisho za utayarishaji. DOWNLOAD / LISTEN HERE  OR  HERE

Ushabiki au Unafiki?

Image
Kila msanii hufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha ya kwamba anafanya kazi nzuri ya kuridhisha mashabiki wake na kukonga nyoyo za kila mmoja atakayesikiliza kazi zake. Msanii hupata furaha pale anapokua na mashabiki sugu ambao wanafagilia kazi zake kiasi cha kua wanaweza kumsaidia kumpigia debe  kazi zake na kusimama kidete nayeye. Hawa mashabiki sugu ndio wale ambao msanii akiacha kazi na itokee wengine waikashif kazi ile au kuiponda basi hao watakua mstari wa mbele kueleze uzuri wa kazi ile na kjaribu kufunika au kutetea kasoro zinazokosewa. Jinsi shabiki anavyotetea kazi ya msanii na kumpigia debe huenda kukamjengea au kumharibia msanii anayeshabikiwa. Kuna mashabiki ambao watajaribu kueleza mtu anayeponda au kukashif kazi ya mtu ya kwamba aangalie ubora wa kazi na yale mapungufu ayapuuze na kuna wale mashabiki ambao ukikosoa tu kazi ya msanii wanayemshabikia basi ni matusi kwenda mbele. Hivi shabiki akimtusi mtu anayekosoa kazi ya msanii, anamjenga au ana m,bomoa? Kwasababu end

NEW MUSIC: Chikuzee Feat Kassim Mganga- NARINGA NAE

Image
Zee la mavuvuzela au kwa harakaharaka CHIKUZEE ni mmoja kati ya wasanii magwiji hapa mkoani. Katika siku za hivi karibuni amekua kimya sana lakini huu hapa ujio wake mpya. Akiachia wimbo huu Chikuzee amesema ya kwamba huu ni ujio mpya na si kurudi tu kushtua lakini amerudi, vizuri na zaidi ya vile alivyokua. Chikuzee amesema ya kwamba huu ni mwanzo mpya tu kwani watu watarajie mambo mengi, tofauti na vile walivyomzoea. Katika wimbo huu ulioandaliwa AM Records ya Tanzania memshirikisha Tajiri wa mahaba, msanii kutoka kuleee kwa Magufuli, Kassim Mganga. DOWNLOAD / LISTEN HERE au HAPA  

Shaa Biggy Anatamani Kufanya Collabo na Kigoto, Alafu ana Maoni Kuhusu Producer Totti

Image
Msanii Sha Biggy kutoka hapa pwani amefunguka na kusema ya kwamba ako tayari kufanya kazi na msanii Kigoto. Akizungumza wakati wa mahojiano katika kipindi cha Kaya Flavaz ndani ya Radio Kaya na Sis Shannie,  Sha Biggy, amesema anakubali kipaji cha msanii Kigoto Mbonde na anaamini wanaweza kutoa kazi nzuri sana endapo watashirikiana watoe wimbo wa pamoja. Akiongea na Shaniez, Shaa Biggy alisema..  “ Kigoto ni miongoni mwa wasanii kutoka kanda ya pwani ninao wakubali zaidi na siwezi kataa nafasi ya kufanya kazi naye”. Shaa Biggy pia alisema haoni ubaya Producer Totti kujitosa katika usanii kwani anaamini iwapo produce anaamini anaweza kuvuna zaidi katika usanii basi hatua yake haina makosa. Vilevile amemsifu Produce Totti kujitosa mzimamzima katika ulingo wa usani na kuwapa wasanii ushindani mkubwa

Dogo Richie Atambulisha Label Yake Na Msanii Wake Wa Kwanza

Image
Dogo Richie ambaye kwa sasa anafanya vizuri saana na wimbo wake wa yoyobah amesema kwamba lengo la kuanzisha label hiyo ni kushughulikia msukukumo ambao amekua akiupata kutoka kwa wasanii wenye vipai wanaohitaji msaada wa kutambulishwa sokoni. Kupitia usemi wake label hiyo ilianza kama group ya whatssap na mwishowe wakafikia katika kiwango cha kum saidia mmoja wa member wa group hiyo kwa kuwa alionyesha uwezo wa hali ya juu wa vocals. Dogo Richie amesema kuwa kwa sasa wameanza na msanii mmoja kwa jina SHYMAN ambaye wanapania kumpa support ya kutosha hadi atoke. ShyMan ni jamaa maarufu hapa mkoani haswaa kwa wasikilizaji wa vipindi  vya mziki wa Afrika Mashariki katika redioza hapa mkoani kwani hua ni vigumu sana kipindi kuisha vila kumskiza amepiga simu redioni. Ni shabiki sugu sa wa mziki wa pwani na mimi binafsi alinishangaza mwishoni mwa mwaka jana wakati Gates Mgenge alipofanya interview ya wasanii sita na producer wawili kwa pamoja, interview ambayo ilikua ya kuf

Collabo yangu Inayofuata itakua na Nameless, asema Dazlah. Na Vipi video ya Bangereba Remix?

Image
Dazlah Kiduche aka KideKide Master amefunguka na kusema ya kwamba collabo inayofuata ataifanya na nguli wa mziki hapa Kenya, David Mathenge au ukipenda Nameless . Lakini hio itakua ni baada ya kufanya single yake solo kani ni mda mrefu sana tangu aachie video ya project yake peke yake. Je hii inamaana ya kwamba Video ya Bangereba Remix ndio imeyeyuka au? Video ya wimbo wa Dazlah , Bangereba remix aliomshirikisha msanii Susumila ni moja kati ya projects ambazo zimekua zikingojwa na mashabiki wengi saana.Ni proect ambayo imetawala vichwa vya habari za burudani kwa takriban miezi sita kwa sasa.Ngoma ilitoka audio ambayo kwa sasa imemaliza takriban wiki tatu sokoni ila swali ni je videoo iliyoahidiwa mashabiki yatoka lini? Kulingana na msanii Dazlah ni kwamba watayarishaji ambao walikua wanatarajiwa kuitayarisha video ya bangereba remix walipendekeza kuwa kwa sasa ingekua bora Dazlah asimame peke yake kwenye video ya single yake mpya ndio baadae atayarishe video ya B

DJ Lenium Apata Bonge La Dili

Image
Ni moja ya malengo ya kila mtu maarufu haswaa katika tasnia ya burudani kuweza kutumia brand au jina lake kupitia jina lake kupata pesa. Mkongwe katika tasnia ya burudani hapa Mombasa, jamaa ambaye anajivunia kuwa katika industry kwa miaka kumi na pia kuwa na tuzo kumi, kiasi cha tuzo ambacho hakuna yeyote hapa mkoani awewahi kufikisha, Daktari Wa Mziki aka Dj Lenium wiki hii alipata bonge la shavu. Wiki hii, kampuni ya teksi ya Uber ilipokua ikitangaza kuanzisha huduma zake Mombasa, pia ilizindua mabalozi wake wawili, ikiwa ni Dj Lenium na Miss Tourism, Tima Keilah . Nilimtafta DJ Lenium angalau anidokezee kama alilambishwa mkwanja wa kiasi gani lakini akadinda kufunguka kiundani na kujibu kwa kicheko akisema "nimelishwa vizuri boss"  

NEW MUSIC: Dula - BABYLON

Image
Anafahamika sana na style yake ya Swahili Reggae hasa baada ya kufanya hit kwa jina BILA WEWE ila Wengi wanamjua kama Triple A , Jina mbalo lilivuma sana enzi zile ALI B akiwa NABS ENTERTAINMENT . Dula ndiye producer aliyemuandalia ALI B nyimbo zake zote alizofanya Nabs Entertainment, kama vile Kadzo na Zungusha . Hio ilikua ni kabla hajaenda nchini Uganda na baadaye Tanzania ambapo aliingilia uandaaji wa filamu na kufanya kazi na magwiji wa bongomuvi kama vile Wolper . Alirudi Kenya na kuanzisha Studio yake mwenyewe, MO TOWN Records. Ikiwa ndio kura za mwakani zishaanza na wanasiasa wapo mashinani kurai wanachi kuwaomba kura , Dula katika wimbo huu anawauliza wanasiasa.. where is our revenue... where is our tax... DOWNLOAD / LISTEN  

Sisi Wanasiasa ni Wanafik Sana, Asema Mike Sonko... Kunani Kwani?

Image
Siku zote, wengi husema kwamba siasa ni mchezo mchafu. Na katika siasa hakuna adui au rafiki wa milele kwani vile vitu ambavyo wanasiasa hufanya mbele ya umma sivyo wanavyovifanya nyuma ya pazia... Yani siasa ni kama sanaa vile, ile uigizaji mwingi na mambo  mengi yanayofanywa na wanasiasa hua ni kwa maslahi yao tu tena kwa mda. Hivi leo kupitia ukurasa wake wa facebook, Seneta wa Kaunti ya Nairobi, Mike Mbuvi Sonko amepost picha akiwa kinyozi akiwa pamoja Seneta wa Kaunti ya Mombasa Hassan Omar na Gavana, Ali Hassan Joho ambaye wengi wanajua ni adui yake mkubwa haswa kuanzi mwishoni mwa mwaka pale Rais Kenyatta alipokuja Mombasa bila kumtaarifu Gavana Joho . Sonko na Joho hurushiana maneno makali mbele ya umma hata nurusa siku moja wazichape  ( Tazama Hapa).  Mombasa, Hassan Omar. Sonko aliambatanisha picha hiyo na maneno: " Sisi politicians ni wanafik sana we are fighting in public but jioni tuko pamoja, we talk together. Wakenya wapendwa musikubali kupiganishwa

NEW VIDEO: Dee Buowy Feat Chapatizzo & CLD - NIPE

Image
Ni msanii wa hiphop na hupenda sana kufuse kiingereza, kiswahili na kimijikenda na track ya ChapChap Remix ambayo aliwashirikisha Susumila, Amoury, Kingstng, Kidis, Johnny Skani, Rojo Mo na Totti ni moja kati ya Track/video za Dee Bouwy ambazo zimepata airplay kubwa. Aliachia audio ya NIPE alyowashirikisha Chapatizzo na CLD na sasa hii ni vdeo yake ambayo ilitayarishwa na Director Edward Martins.

Eti Kenyan Men Are Much Cheaper

Image
Wanawake wengi wa hapa nchini wameonekana kuwapenda sana wanaume kutoka nchi za nje. Wanawake wengi ambao wamekua na mahusiano na wanamume kutoka nchi za nje wamesifu sana wanaume kutoka Africa Magharibi hususan Nigeria   wakidai kua wanajua kudekeza na kupetipeti naukija kwa pochi usiulize, kwani wanajua kutunza wanawake wao na hela. Wanaija wenyewe hivi majuzi walifunguka na kusema si eti hao wanajua kupetipeti lakini wanawake wa Kenya ni rahisi sanaaa. yani kuwatongoza na kumgharamia mwanamke wa Kenya ni rahisi kama kutandika mkeka vile yani wanauwake wa Kenya hawana thamani. Wapo walionekana kuunga mkono kauli hio haswa baada ya kusambaa video mitandaoni ya mwanamke kwa jina 'shiro' alikonekana akijipendekeza na kucheza kwa mahaba akimtongoza mwanamme flani ivi ambaye alikua akiongea na asili nzima ya kinigeria. Wanawake wengi hawajapendelea kauli hii ya kwamba wanawake wa Kenya ni rahisi na wamekua wakilalamika sana. Leo katika Kipindi cha MwakeMwake kinachoendes

Hiki Ndicho Kitakachokua Kinatokea Kila Alhamisi Hapa Mombasa

Image
Wasanii wengi hapa mkoani wamekua wakitamani sana angalau kama wana,launch video zao basi iwe launch kubwa, angalau ihudhuriwe na washikadai wengi wa mziki sana sana mashabiki na wasanii wenzao angalau kuwapa support. Imekua kitu kigumu kufanyika kwani hata kuna wakati Gates Mgenge alikua akifanya hivyo mbeleni katika event iliyokua ikiitwa Showbiz Wednesday lakini baadae ikasitishwa. Kumekua na pilkapilka nyingi watu wakitamani wapate tena plartform ya pamoja ambayo watakua wakifanya uzinduzi kama sehemu zengine, mfano Nairobi wanavyofanya. Hatimaye plartform imetengeneza. Kuanzia Alhamisi hii na kila Alhamisi inayofuata wasanii watakua wanaachia video zao mpya katika ukumbi wa Dans Lounge-Valencia Inn Mombasa. DJ Lenium atakua aki,host event hio na kila wiki kutakua na Dj tofauti watakao kua wanatumbuiza. Alafu kutakua na redcarpet ambapo watu watakua wanapiga picha kwa hisani ya Explode Africa Photography. Johnny Skani na crew yake ya Pungwe, Pwani Tv pia watakuwepo k

BabTale Ajitokeza Kumsaidia Chidi Benz

Image
Rapper mkongwe na mkali wa hiphop bongo amegongwa vichwa vya habari baada ya yeye kuonekana jinsi mwili wake ulivyoisha na kukiri ya kwamba hali yake ya afya kwa sasa ni mbya na anahitaji msaada ili arudi kama zamani na apate mafanikio kama ya vile ya Diamond. Hatimaye ni kama ule msaada ambao alikua anatamani sana Chidi Benz ukawa umemfikia. Hio ni baada ya manager wa Diamond ambaye pia ni manager wa TipTop Connection, Babu Tale kujitokeza na kusema ya kwamba ameamua kumsaidia Chidi Benz. Tale kupitia Instagram alipost video akiwa na Chidi Benz. Tale amepost : Mungu nisimamie ni ngumu ila naamini tutashinda #ukukwetu . katika video hio ambayo Chidi Benz ameonekana ni mwenye furaha akisema "Mungu tusimamie, tujaalie, mjaalie Tale, nijaalie na mimi, tunaomba mengi, tutakua na vingi, tutaenda sehemu nyingi, tutafanikiwa..". Wengi wameonyeshwa kufurahishwa na hatua hio ya BabTale kumsaidia Chidi ila si wote walipokelea habari izo vyema kwani mfano msanii Yo

Izzo Bizness Feat Barnaba & Shaa-USIJIOVADOZ

Image
Mwishoni mwa wiki jana Chidi Benz katika interview na Clouds Tv alionekana alivyokondamana na akieleza jinsi anavyoteseka na anahitaji msaada. Chidi Benz amehusishwa sana na utumiaji wa madawa ya kulevya haswaa pale alipokamatwa uwanja wa ndege na heroine na bangi. Wengi wakielekeza kidole cha lawama utumiiaji wa madawa ya kulevya shida anayopitia Chidi Benz, Izzo Bizness amewashirikisha Shaa na Barnaba katika hii track ambaye wanaongelea kula bata. Si eti wanakataza watu wajistareheshe lakini cha msingi ni kwamba mtu awe na limits... Ebu iskilize. DOWNLOAD / LISTEN

NEW MUSIC: T.I.D Feat Dully Sykes & Joh Makini- CONFIDENCE

Image
3kings , kama walivyojiita katika ngoma hii iliyotayarishwa na Nusder . Ni Khalid Salum Mohamed aka TID akiwa amewashirikisha mkongwe wa bongofleva, hitmaker wa Shikide - Dully Sykes na mkali wa hiphop ambaye kwa sasa ndio jamaa anayepeta sana katika anga za hiphop Afrika Mashariki, hitmaker wa Don Bother-Joh Makini aka Mwamba wa Kaskazini . Kama kuna collabo za mwaka basi hii ni moja wapo. DOWNLOAD/LISTEN HERE

Chidi Benz Anahitaji Msaada

Image
Msanii mkongwe wa hiphop, Rashidi Abdallah Makwiro   aka Chidi Benz amejitokeza na kusema ya kwamba hayuko sawa kwa sasa na anahitaji msaada. Chidi Benz ambaye wengi wamekua wakisema anatumia madawa ya kulevya, madai ambayo yalitiliwa mkazo pale aliponaswa na madawa ya kulevya aina ya heroine na bangi mwaka 2014. Mwaka huo huo Dully Sykes akijaribu kumsaidia Chidi arudi kwenye game alimkutanisha na AY na Diamond wakafanya ngoma- MPAKA KUCHE. Diamond alikiri ya kwamba Chidi Benz alimsaidia kutoka kwa aimuomba collabo alipokua chini na Chidi Benz hakumuonyesha nyodo na wakafanya "Nalia na Mengi" bila kumuitisha hata sumni. Lakini ni kama msaada huyo haukudumu kwa mda mrefu. Tusonge mbele kidogo... mwishoni mwa wiki jana, Chidi Benz akihojiwa katika Clouds TV alishtua wengi kwani jinsi alivyokonda si mchezo. Chidi alisema ya kwamba uwezo wa mziki bado anao ila wale wadai wanaoshikilia mziki wamemtupa. Chidi alisema ya kwamba angekua kwenye game kwa sasa wana

NEW MUSIC: Raymond-KWETU

Image
Ni talanta ambayo ilikua katika malezi ya TipTop Connection ila sasa amekua msanii wa pili kusajiliwa katika label ya WCB ya Diambond Platnumz baada ya Harmonize. Raymond alitambulika mwaka 2011 alipoebuka mshindi  katika shindano la Freestyle mjini Mbeya ndipo akasajiliwa na TipTop Connection ambapo alipata kuonekana sana katika show nyingi za Madee na TipToP Connection . Ukaribu wa TipTop Connection na WCB ndio uliowezesha Raymond kujiunga na WCB na hii ndio track yake ya kwanza katika WCB akimwelezea mschana anayempenda jinsi maisha ya kwao ya umaskini yalivyo. DOWNLOAD / LISTEN HERE

Hii ndio Sababu Iliyowafanya Wasojali Band na Kelechi Africana kuiga wimbo wa Hello ya Diamond Platnumz

Image
Watu wengi wametoa waoni yao kuhusu wimbo wa Nitalia Nawe wa Wasojali Band na Kelechi Africana, haswaa baada ya kuachiwa kwa video ya wimbo huo. Japo kua watu wameipa shavu video hio kwa jinsi ilivyoandaliwa na kusema iko kiwango cha juu zaidi na tofauti na video zingine walizotangulia kufanya Wasojali Band   wengi wameonekana kukemea wimbo huo wakisema ya kwamba wamecopy beat ya wimbo wa Hello wa Diamond Platnumz. Nilimtafuta manager wa Kubwa Entertainment, Athman Baba aka Babaz ambaye ndiye anayesimamia Wasojali Band na Kelechi Africana kumfikishia malalamishi hayo ya mashabiki na kujua ilikuaje wakaamua kutumia beat ya wimbo mwengine wakati Producer Noizer aliyetayarisha Nitalia Nawe anauwezo mkubwa na ubunifu wa hali ya juu na hashindwi kutengeneza kitu halisi. Athman Baba alisema ya kwamba mwanzo kabisa angependa kidole cha lawama kisielekezwe kwa Producer Noizer kwani maelekezo yote ya project hio yalitoka kwake... Babaz alisema ya kwamba aliposikia wimbo w

Queen Renee Awakilisha Pwani katika Kenya Culture & Fashion Show Nchini Ujerumani

Image
Irene Njeri aka Queen Renee ni msanii kutoka hapa Mkoani maeneno ya Mtwapa . Ni msanii wa kike  ambaye kufikia sasa ana nyimbo 12 kibindoni ambazo ziko kwenye album zake mbili. Akiachia video ya Champaign hapo mwezi jana, Renee alifunga safari kuelekea nchini Ujerumani , si kwa matembezi, masomo au kazi bali kuwakilisha Pwani na Kenya kwa ujumla katika maonyesho ya Kenya Culture And Fashion Show . Aliwakilisha Pwani vilivyo na hizi ni picha za maopnyesho hayo ambayo Renee alihudhuria. Renee pia amedokeza ya kwamba wiki ijayo anaanza media tour kuendelea kutambulisha wimbo na video ya champaign...itazame