Mlezi Wa Models Wengi Maarufu Aeleza Kwanini Models Wengi Hufeli

Dya Candy si jina geni katika sanaa ya uana mitindo. Kampuni yake ya Fuschia Creativity ambayo kwa sasa ni clotheline na beauty world ndio kampuni ya kwanza mjini Mombasa ku,manage wanamitindo. Sandra Shiqo, Ruthalia Michaels, Anita Nzaro, Talal, Catherine Mage na Catherine Ariana ni miongoni mwa wanamitindo maarufu ambao wamewahi kupitia mikononi mwake kuwafunza kazi ya uanamitindo.

Ni warembo wengi na vijana wengi wamekua wakijaribu kua wanamitindo lakini wamekua wakiacha kazi hio kwa kua wanaona ya kwamba haina mwelekeo mzuri, wengi wakisema ya kwamba wananyanyaswa kimapenzi na wengine wakisema ya kwamba malipo yako chini hivyo basi haiwezi kua kama kazi, je shida iko wapi, mbona wengine wanadumu katika sanaa hii na kuweza kujikimu na kujtengenezea majina makubwa?
Mwanamitindo huyu gwiji anasema ya kwamba wanamitindo wengi wanaochipukawamekua wakibuma baada yam da mfupi kwa kua hawajui wanachokifanya na nasaha nayowapa ni kwamba  wanafaa wawe wakifanya kazi na mtu anayeelewa vizuri maswala ya mitindo na burudani kwa undani.
Dya Candy ambaye kwa sasa anastawisha kampuni yake katika vipodozi na mavazi anawania  taji la FACE OF MOMBASA katika tuzo za VibeCity Awards Mombasa ambazo zitafanyika Jumamosi hii katika ukumbi wa Azura Lounge. 
Bado washiriki wa tuzo za kifahari wanabigiwa kura na wanaopiga kura wanapata nafasi ya kujishindia airtime ya kati ya kshs.100 na kshs.1000 ( Kuna washindi 10 kila siku)... kupiga kura ni HAPA

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele