CHIKUZEE AUNDA KUNDI LA MZIKI



Msanii Chikuzee ni mmoja kati ya wasanii tajika kutoka kanda ya pwani ya Kenya. Waakati alipoachia collabo mbili na msanii Susumila mashabiki wengi walitamani sana wawili hao waungane na kuwa kundi moja ila uhusiano wao haukuduma sana kuanzia 2015 wawili hao walianz kua na tofauti baina yao.
CNew naye alikua pamoja na msanii Fat S  na 35% katika kundi lao la RBeez,  enzi hizo CNew alikua akijiita Njemba Boy.  Pia nalo ni kundi ambalo lilikuja vunjika baadae. Miaka imesonga sasa na wawili hao, Chikuzee na CNew katika siku za hivi karibuni wameonekana wakiwa na ukaribu sana na wameweka wazi ya kwamba, pamoja na Producer B.I wamekuja pamoja na kuunda kundi kwa jina DOSSARI INTERNATIONAL.
‘Tumeunda kundi na mtindo wetu wa mziki unaitwa TamTam Flevaz. Si kwamba ni kundi ambalo linatufunga sana bali kila mtu bado ana uhuru wa kufanya solo projects zake lakini tukiwa pamoja ndio Dossari International. Kuna kazi nyingi ambazo tayari tushazikamilisha  nay a kwanza ndio yumeiachia hivi sasa na inaitwa DUNIA NZIMA.’ CNew ameeleza hayo huku akiahidi mashabiki wangojee kazi nyingi nzuri kutoka kwao  kwani anaamini huu mwaka ni wakati wa kundi hilo kutamba. Itazame video ya kundi hilo ambalo linatarajiwa kuteka nyoyo za wengi mwaka huu hapa chini….

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele