Susumila Kufunga Ndoa Mwezi Wa Aprili
Kando na kufanya kazi nyingi na kubwa mwaka wa 2016, moja ya vitu vilivyoongelewa sana
kumhusu ni kutalakiana na aliyekua mkewe, Kibibi
Salim ambaye walikua wameoana kwa miezi 11 tu.
Miezi mitano sasa
baada ya Susumila kutalakiana na muigizaji Kibibi Salim ambaye walikua wamejaaliwa
mtoto mmoja, mdokezi wetu wa kuaminika ametudokezea ya kwamba Susumila anajipanga kufunga pingu za
maisha mwezi wa Aprili.
Mdokeni wetu ambaye ni rafiki wa karibu sana wa msanii huyu
amedinda kumfichua bibi harusi mtarajiwa
ila ametudokezea tu ya kwamba mrembo
huyo aliyeteka moyo wa Susumila ni mtoto
wa mwanasiasa mmoja tajika kutoka eneo la pwani na harusi ya wawili hao
haitafanyika nchini Kenya. ‘Zile safari
nyingi ambazo Susumila amekua
akisafiri zimekua si za matembezi tu bali ni za matayarisho ya harusi yao.
Harusi yenyewe imepangwa kuhudhuriwa na watu 35 tu. Watu wote hao watagharamiwa
usafiri na malazi kkatika nchi ambayo kutafanyika harusi hio.’ Mdokezi wetu
ametueleza. Nilipomtafuta Susumila
kuthibithisha uvumi huu alinijibu tu kwa kicheko na kukataa kufunguka.




Twasubiria
ReplyDelete