Azidisha Mbwembwe Baada Ya Kutoka Mafichoni



Ni mwezi jana tu ndio msanii Professa Nasha aliweza kuachia kazi yake mpya baada ya kua mafichoni kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja baada ya kufumaniwa na mke wa mwanasiasa maarufu hapa pwani. Stori hio iko >> HAPA.
Baada ya kurudi rasmi katika mziki, Professa Nasha ameamua ni kazi baada ya kazi kwani baada ya mwezi tu tayari ameandaa video mpya. ‘Nilikua nimewamiss mashabiki wangu na najua walikua wanakosa sana kazi nzuri kutoka kwangu lakini hio ni zamani kwa sababu nimerudi kuwaridhisha na nawaahidi kuwapa kazi nzuri bila kuchoka. Naelewa ya kwamba si rahisi kurudi nilipokua baada ya kimya cha mwaka mmoja lakini najibidisha kwa ajili ya mashabiki wangu.’ Nasha amesema hayo wakati alipokua anazindua video yake mpya ya ULIENDA WAPI iliyoandaliwa na DreamLand Music. Kua wa kwanza kuitanza video hiyo hapa chini....

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele