Fat S Afunguka Kuhusu Mziki, Kuuza CD, Mayai Na Diss Ya Dogo Richie



Wiki hii msanii Fat S ameongelewa sana baada ya kusemekana ya kwamba katika siku za hivi karibuni amekua akionekana akiuza mayai katika kivukio cha Likoni.
Kelvin Jilani / Mtu Bei alifanikiwa kumpata Fat S na wakawa na mahojiano ambayo Fast S alifunguka mengi kuhusu yeye mziki na biashara zake. Katika mahojiano hayo,  Fat S alifunguka na kueleza ni jinsi gani amekua akiifanya biashara yake ya kuuza CD pale Ferry na inamuingizia pesa kiwango gani.
‘Unajua mimi ni msanii  na mimi ni kioo cha jamii. Kila kitu ninachofanya hua nafanya kwa ajili ya kufunza jamii, kwa hio ple ninapo uza Cd ferry naonyesha jamii ya kwamba nategemea kazi yangu na kipaji change ndio kinanilipa. Mimi sifanyi  mziki ubishow bali nafanya kama biashara. ‘ Fat S amesema huku akisema ya kwamba wale wasanii wengi ambao wamekua wakimcheka ndio ambao hawana lolote kwani ni njaa na kukosa pesa ndio wanajua
‘Msanii anayejua analofanya hawezi akaingia studio na kutoa pesa zake akaimba watu. Dogo Richie alijua kuna wasanii vigogo ndio akaamua kuwataja ili apate kiki. Dogo Richie amepata umaarufu kwa kuwaimba wenzake  ila asilojua ni kwamba amejijengea chuki.’ Fat S amefunguka. Je ana beef na Dogo Richie kwa kumuimba katika nyimbo mbili kama mfano wa jinsi mziki unavyohangaisha wasanii? Na vipi kuhusu yeye kuuza mayai katika kivukio cha Likoni? Msikilize alichokisema kuhusu hilo >>  HAPA

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele