Kundi Linalojihusisha Na Mziki, Uhamasisho na Biashara Kwa Vijana


NewLife Music  si kundi tu la mziki bali pia ni shirika linalojihusisha kuhamasisha vijana kuishi maisha yenye muelekeo katika jamii.
Waanzilishi wa kundi hili, Kally D na Baracka J.O hawafanyi mziki wa injili tu ila wanahubiri amani haswaa wakati huu nchi inapoelekea kufanya uchaguzi. Katika kuhubiri kwao, wanaowalenga sana ni vijana kwani hao ndio hutumika sanasana na wanasiasa na bila uhamasisho mzuri husababisha madhara makubwa si kwa vijana wenyewe tu bali kwa nchi nzima kwa ujumla.
Kimziki  kwa sasa Kally D ameachia video yake ya NISHIKE na inaendelea kufanya vizuri na kuanzia mwezi ujao tutakua tunatayarisha video ya wimbo mmoja wangu. Ameeleza Baracka J.O ambaye ameendelea kusema ya kwamba wanajihusisha na biashara ya mavazi na wako na clothingline  ( New Life Music -  NLM) ambayo wanaipangia kuifanyia uzinduzi mkubwa hivi karibuni.
Tunakaribisha wasanii wenzetu wa injili wajiunge nasi. Atakayetuma maombi atakaguliwa kulingana na utaratibu wa panel inayoongozwa nab boss Bizzoh na iwapo mtu atapitishwa basi atajiunga nasi na kufanya kazi nasi. Amemalizia Kally D.

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele