Otile Brown Atengana Na Dr Eddie (DreamLand Music)



Wiki moja tu baada ya manager wake kufuta video zake katika mtandao wa Youtube,  hitmaker wa Dejavu,  Otile Brown ametangaza kuachana na management ya Dreamland Music inayomilikiwa na Dr Eddie.
Wakati video zake ilipoondolewa katika mtandao wa Youtube,  akiongea na mtandao mmoja maarufu Afrima Mashariki, Otile Brown alikiri na kusema ya kwamba kuna tofauti  imeibuka baina yake na manager wake ila anatarajia ya kwamba watasuluhisha katika siku za hivi karibuni. Ila inaonekana tofauti zao zimeshindwa kusuluhishwa kwani mapema hii leo kupitia mitandao ya kijamii, Otile Brown ametangaza ya kwamba hayupo tnea chini ya uangalizi wa DreamLand Music.
Japo  hakueleza  kilichopelekea wawili hao kutengana, bali ameandika na kusema ya kwamba hayupo tena Dreamland Music na akahakikishia mashabiki wake ya kwamba hatowaangusha. Itakumbukwa ya kwamba, kabla video zaek kufutwa katika mtandao wa Youtube, Otile Brown ndiye msanii kutoka Pwani ambaye alikua na views nyingi katika video zake kwani hakuna video yake hata moja ambayo ilikua na views zilizopungua 300,000.

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele