Polisi Wapiga Breki Mkutano Wa Hadhara Wa ODM
Chama cha ODM kimepigwa breki kufanya mkutano wa hadhara
ambao ulikua umepangwa kufanyika hii leo katika uwanja wa Mvita.
Kulingana na barua aliyoandikiwa mwenyekiti wa chama hicho
tawi la kaunti ya Mombasa kutoka kwa mkuu wa kituo cha polisi cha Makupa ni
kwamba chama hicho kilikosa kuomba ruhusa ya kuandaa mkutano huo masaa 72 kabla
ya siku ya mkutano kama inavyostahili.
Vilevile, mkutano wa hadhara wa chama cha Jubilee uliohudhuriwa na Uhuru Kenyatta uliofanyika katika uwanja wa
Tononoka pamoja na mkutano wa maombi wa prophet Owuor imetumia usalama mkubwa
hivyo basi kupunguza uwezo wa polisi kupeana usalama katika mkutano mwengine wa
hadhara.
Comments
Post a Comment