Upinzani Uache Unafik, Asema Rais Uhuru Kenyatta



Rais Uhuru Kenyatta amesema ya kwamba chama cha Jubilee ndio chama pekee ambacho kinapaswa kuongoza nchi hii.
Akiongea katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho katika uwanja wa Tononoka, rais Uhuru alisema ya kwamba Jubilee ni chama ambacho kiliundwa kwa nia ya kuunganisha wananchi kwa nia ya kuwafanyia wananchi kazi ili kufanya miradi na maendeleo  ambayo yataboresha maisha ya mwananchi wa kawaida.
Uhuru alisisitiza ya kwamba Jubilee pekee ndio suluhisho la maendeleo kwa wakaazi wa pwani kwani mirandi  iliyofanya serikali ya Jubilee kwa wapwani haikuwahi kufanywa na serikali zilizotangulia. Akitoa mfano wa  maendeleo yaliyofanyika katika eneo la pwani, rais Uhuru alisema ya kwamba tangu serikali yake iingine uongozini, imewapatia wananchi 200,000 hati miliki za mashamba katika  eneo la pwani tu  katika mda wa miaka minne ambayo amekua uongozini.
‘Tukiomba kura hatukulia lakini tulikua tunajua ya kwamba wapwani wamedhulumiwa na tukaona ni sawa wapwani watekelezewe… wanasema ni haki yenu serikali kuwafanyia maendeleo lakini mbona serikali zilizotangulia hazikufanya hivyo? Ni kwa sababu serikali ya Jubilee ni serikali yenu ndio maana inawatekelezea haki yenu.’ Rais Kenyatta aliyasema hayo huku akieleza ya kwamba serikali yake imetumia zaidi ya kshs bilioni 30 katika ujenzi wa barabara katika eneo la pwani.
Akimalizia, rais alisema ya kwamba wapinzani waache unafiki na matusi kwani yeye ana simama kideti na kazi aliyofanya katika miaka minne kazini sio kama baadhi ya magavana wa upinzani wanaojipiga kifua wakati hawawezi eleza jinsi walivyotumia bilioni 40 zilizogawia kaunti zao

Comments

Popular posts from this blog

ThrowBackTrack.... MACHUNGU - Daddy Sele