Huwezi Fanya HipHop Kama Wewe Si Genius, Asema MamaLao
Mkali wa uzito wa mistari na kufoka, Mamalao ambaye kwa sasa anafanya vizuri na track yake ya SUMU KALI ameweka wazi kuwa kilichomfanya akakita mizizi kwenye Hip hop ni kwa sababu ya msukumo wa kipaji huku sababu nyingine ikiwa ni kwamba wasanii wengi wa kike wameogopa kufanya hip hop hivyo ameamua kufanya hip hop ili kuwa mfano kwa wasanii wa kike. ''kwanza mimi nasema mziki wa hiphop ni mziki unaofanywa na watu wenye akili nyingi za ziada kwa sababu ukikaa chini ukiskiza hiphop utaskia maneno ambayo yanamgusa mtu kwa hivyo mtu anayefanya hiphop ni genius kwa kua anahitaji akili nyingi sana kuandika' '... amesema MamaLao Mamalao amewapa changamoto wasanii wa kike ya kujitokeza kwa wingi kufanya hip hop ili asiwe peke yake kwenye industry ya mziki wa huo. "yaani mimi nawambia wajitokeze kwa wingi maana endapo watanifanya mimi sina competition ya kutosha hapa coast watanifanya mimi mzembe" MamaLao pia amefunguka na kusema kwamba yuko single...je,...